KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Wednesday, 22 April 2015

SERIKALI YARIDHISHWA NA MAONESHO YA MADINI YA VITO

SERIKALI imesemasema kuwa imeridhishwa na maonyesho ya madini ya vito yaliyoandaliwa na  jumuia ya wafanyabiashara wa madini nchini Tamida,kutokana na kuonyesha mafanikio makubwa  yakiongozwa na madini ya Tanzanite.
Waziri wa Nishati  na Madini,George  Simba Chawene,ameyasema hayo leo alipokuwa akifungua maonyesho ya nne ya madini ya vito yanayoshirikisha wauzaji, wanunuzi wakubwa wa madini hayo ulimwenguni .
Chawene,amesema kuwa hivi sasa serikali ipo katika hatua za uimarishaji wa kiutengenezaji madini  ukataji wake na uchongaji  hivyo kuyauza yakiwa yameongezewa thamani na kutoa ajira  nyingi tofauti na awali ambapo yalikuwa hayatoi ajira hizo kutokana na kuuzwa yakiwa ghafi.
Amongeza kuwa serikali ipo katika hatua za mwisho kutengeneza kituo kikubwa cha kuuzia madini ambapo kutakuwepo na Hotel, maduka na ofisi za mamlaka ya mapato TRA, na uwanja wa kutua Helkopta  na hivyo kuondoa ulanguzi wa madinin na hivyo kuongeza pato la taifa sanjari na kuondoa urasimu uliokuwepo wakati wa mauzo ya madini.
Pia serikali itaweka  vituo maalumu vya ukaguzi  kwenye machimbo ya Tanzanite,ili kudhibiti wizi sanjari  na kurejesha  utaratibu wa kujenga ukuta uliokuwepo kwenye machimbo hayo  ambao ulibomolewa na baadhi ya watu wenye nia mbaya ili waweze kutorosha madini hayo kwa urahisi ,pia kuimarisha  ,utolewaji wa vitambulisho .
 
Ameongeza kuwa utoroshaji wa madini unaofanywa na watanzania ambao wamepewa leseni za kuuza na kununua madini umepungua kutokana na udhibiti kuimarishwa.
Amesem,a miaka miwili iliyopita Tanzania ilipata dola milioni 38 za kimarekani kutokana na mauzo ya Tanzanite, huku Kenya ikipata dola milioni 100 kutokana na mauzo ya Tanzanite, na India ilipata dola milioni 300.

No comments:

Post a Comment