KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Thursday, 30 April 2015

SIMBACHAWENE AVUNJA MKTABA NA SELCOM

WAZIRI wa Nishati na Madini, George Simbachawene,  amevunja mkataba wa uwakala wa Kampuni ya Selcom kutokana na mitambo yake ya kuuza Luku kuwa na matatizo ikiwemo matatizo ya kisheria katika kulipa kodi.
Simbachawene alitoa kauli hiyo baada ya kulizwa swali na wandishi wa habari kuhusu usumbufu wanaoupata wateja kila inapofika mwishoni  mwa mwezi wanapotaka kununua huduma hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutembelea miradi ya ujenzi ya vituo vya kutoa huduma ya nishati hiyo, Waziri huyo alisema kuna kampuni mbili zilishinda zabuni ya kufanya kazi hiyo ya kuuza umeme kupitia mashine za Luku ambazo ni Selcom na Max com.
“Nakuagiza mkurugenzi, kuiondoa kampuni hiyo na atafutwe mtu mbadala ambaeye ataweza kufanya kazi hiyo na sio lazima afanye yeye amabaye ameshindwa kutoa huduma kwa wananchi.
Simbachawene alisema anamtaka mkurugenzi huyo wa Tanesco akamilishe mchakato huo haraka kwani tangu aingie katika wizara hiyo ni mara ya tatu kusikia malalamiko hayo ambayo yanasabishwa na kampuni hiyo, jambo linalowafanya wananchi washindwe kununua umeme na mwisho inayolaumiwa ni Tanesco na Serikali.
“Hali hiyo inatokana na yule anayesimamia mauzo na kuuza umeme mitambo yake ina matatizo lakini zaidi kuna masuala ya kiufundi pia kuna matakwa ya kisheria kwamba lazina alipe kodi lakini kwa sasa wananchi waende kwa wakala wa Max com amabaye mitambo yake haina matatizo,”alisema Simbachawene.
Simbachawene alimtaka Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco kulishughulikia suala hilo baadala ya kumuacha aendelee kuchezea huduma hiyo muhimu kwa uchumi wa nchi.
Akizungumzia Miradi hiyo, Waziri, alisema baadhi ya miradi inayo endelea kutekelezwa ni pamoja mradi wa Mbagala Megawati 100, Kurasani megawati 50, Gongolamboto Megawati 50, Kipawa Megawati 180 na Transmission line ya kuunganisha vituo hivyo.
Simbachawene, alisema kazi zote hizo zinaendelea, baadhi zimekamilika na nyingine zitakamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu.
Aliongeza kuwa kukamilika kwa miradi hiyo kutalifanya jiji la Dar es Salaam kuwa miongoni mwa majiji yenye mfumo imara wa umeme katika Bara la Afrika.
Simbachawene, alisema kukamilika huko kutawahakikishia umeme wa uhakika na kuondoa tatizo la kukakatika mara kwa mara kwa umeme katika jiji hilo.
Mkukurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Felchesmi Mramba, alisema licha ya matatizo hayo pia wamepokea maelekezo kutoka Malaka ya Mapatao Tanzania (TRA), ya kuitaka Tanesco kufuta mkataba kati yake na Selcom, jambo ambalo wameanza kulifanyia kazi tangu juzi.
 “Tatizo la kukosekana umeme halitokani na Tanesco bali linatokana Selcom hivyo tayari tumekwisha mkatia huduma hiyo kutokana kwa hiyo hatunaye kwa maana hiyo serikali imevunja mkata na serikali kutokana na kukwepa kulipa kodi,”alisema Mramba.

No comments:

Post a Comment