KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday, 1 May 2015

TANESCO YAKANUSHA TAARIFA ZA MITANDAONI KUHUSU KUKOSEKANA KUKU


Mkugenzi Mtendaji wa Tanesco, Felchesmi Mramba

SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco), limewataka wateja wake kununua huduma ya umeme wa LUKU kwa kutumia Wakala wa Maxmalipo nchi nzima, Benki ya CRDB na NMB kila zilipo.
Kauli hiyo hiyo imetolewa na Meneja Uhusiano wa Tanesco, Adriano Severine, baada ya Kampuni moja ya simu za mikononi kusambaza ujumbe unaosema: Ndugu mteja huduma ya LUKU haipatikani kwa sasa kutokana na shida iliyopo upande wa washirika wetu, tafadhali tembelea wakala wa Tanesco kununua umeme wako.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, Severine, alisema kampuni iliyofasambaza ujumbe huo ina matatizo ya kimkataba na Tanesco.
Meneja Uhusiano huyo, alisema ili Wateja wenye Akaunti ya Benki ya CRDB, wapate huduma hiyo watapaswa kupiga *150*03# na wale wa NMB, wapige *150*66#, kisha wafuate maelekezo.
“Tunaomba wateja wetu watumie njia hizo ili kujipatia huduma hiyo,”alisema Severine.
Severine, alisema pia wateja wa NMB wanaweza kununua LUKU kupitia NMB Mobale, sehemu nyingine ambazo mteja anaweza kununua LUKU ni katika Ofisi zote za Tanesco zilizoko nchi nzima ambazo zitafanyakazi mpaka siku za Jumapili.
“Tanesco inawaomba wateja wake kuzipuuza taarifa za kukosekana kwa huduma ya LUKU kwa baadhi ya Mawakala, tunakanusha taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao kuhusu kukosekana kwa huduma hiyo kuwa si sahihi bali huduma hiyo inapatikana kwa kutumia Maxmalipo nchi nzima, CRDB na NMB kwa wateja wenye Akaunti na benki hizo,”alisema Severine.
Aliongeza kwa kusema kuwa kwa upande wa mitandao ya Simu wateja wanaweza kununua umeme kupitia M-Pesa na Airtel Money.
Aidha, aliwataka Mawakala ambao hawawezi kuuza umeme wasiliane na Tanesco kwa mujibu wa mikataba yao na si vinginevyo.

No comments:

Post a Comment