KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday, 28 April 2015

TUME YA HAKI ZA BINADAMU YATOA MAFUNZO KWA WANDISHI WA HABARI KUHUSU HAKI ZA BINADAMU



KATIBU Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu, Mary Assay, amezitaka Wizara zote kuufanyia kazi Mpango Kazi  wa kitaifa wa miaka mitano unaoanzia mwaka  2013 hadi 2017 kwa ajili ya uimarishaji haki za binadamu nchini kupitia malengo yake.
Assay, alitoa kauli hiyo, wakati wa mafunzo ya siku moja ya kuwajenge uwezo waandishi wa vyombombali vya hari jinsi ya kuripoti taarifa zinazo husu haki za binadamu, yaliyofanyika jijini Dar es salaam leo.
 “Unajua uelewa wa masuala ya haki za binadamu nchini bado ni mdogo, haswa maeneo ya vijijini ikiliganishwa na maeneo ya mijini,”alisema.
Assay, alisema malengo hayo ni kuboresha hali sasa ya haki za binadamu kwa wananchi wote, hususani masikini, wanyonge, jamii ya walio katika mazingira hatarishi na waishio pembezoni mwa nchi.
Alisema mpango huo utaongeza ufikikaji, kuaminika, uwajibikaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na taasisi nyingine za kitaifa za haki za binadamu kwa kuziimarisha na kuzipanua kiuwezo.
 Aidha, mpango huo umebainisha haki 23 zilizoko katika makundi manne ya ki-mada kama maeneo ya kipaumbele katika kuimarisha ukuzaji na ulinzi wa haki za binadamu nchini.
 Assay, aliyataja makundi hayo kuwani Haki za kiraia na kisiasa, Kiuchumi, kijamii na kiutamaduni, Makundi yenye mahitaji maalumu na kuimarisha taasisi na masuala yaliyopo.
 Aliongeza kwa kusema kuwa tume hiyo ya haki za binadamu na utawala bora kwa kushirikiana na Wizara ya Katiba na Sheria na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali itafuatilia kwa karibu utekelezaji wa Mpango huo.
 Awali akizungumzia mafunzo hayo, Mratibu wa Mpango huo, Laurent Burito, alisema tume imeamua kuwapatia mafunzo wandishi wa habari kwa vile anaamni watakapo uelewa vizuri itakuwa rahisi kwao kufikisha ujumbe uliyo sahihi kwa wananchi.
 Serikali ya Tanzania iliamua kuanzisha mchakato huo kwa mujibu wa mapendekezo ya Azimio la Viena la mwaka 1993 na Programu yake ya utekelezaji katika kila serikali duniani.

No comments:

Post a Comment