Mwandishi wetu, Mwanza
WAMILIKI
wa redio za jamii wametakiwa kujenga taswira njema za redio zao ikiwa
wanataka redio zao zitamanike na kutumiwa na wadua mbalimbali wa
maendeleo nchini.
Kauli
hiyo imetolewa na Mwezeshaji wa warsha ya Viongozi wa vituo vya redio
jamii Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi ya kuwawezesha wajasiriamali wadogo
na wakati (ASMET), Ramadhan Ahungu.
Akizungumzia
malengo ya warsha hiyo na madhumuni yake alisema kwamba kuwapo kwa
mpango wa biashara ndani ya redio hizo hakutakuwa na maana kama
wasipozingatia ujenzi wa taswira utakaowafanya wadau kuvutiwa na redio
hizo.
Alisema
kuna umuhimu wa suala hilo kwani kusipojengeka kwa mahusiano bora kati
yake na jamii, watu binafsi na taasisi za kiraia zenye malengo tofauti
katika kuhudumia wananchi, redio hizo hazitakuwa na biashara ya kufanya.
Ahungu
pamoja na kusifia mtindo uliotumika kuwezesha redio hizo kuandaa
mipango kazi ya biashara yenye lengo la kusimamia masoko na fedha
alisema warsha imefanikiwa kuwaweka karibu zaidi na wadau wamiliki wa
vyombo hivyo.
Warsha
hiyo ni hitimisho ya awamu ya kwanza kwa ufadhili wa mradi wa Shirika
la Maendeleo la Sweden (SIDA) wa kuzipa uwezo redio za jamii katika
matumizi ya Tehama na mawasiliano inayoratibiwa na Shirika la Kimataifa
la Elimu Sayansi na Utamaduni UNESCO iliyofanyika katika kituo redio cha
Sengerema Telecentre mkoani Mwanza.
Alisema
katika warsha hiyo wamiliki hao walijifunza uandaaji wa mipango ya
biashara, kutunza fedha, utafutaji masoko, uhakiki wa mipango ya
biashara na vipindi vya redio kwa lengo la kuona namna ya kuvifanya
kuleta biashara.
Naye
Meneja wa kituo cha Redio Jamii Kahama FM ya Shinyanga, Marco Mipawa
akizungumzia mafunzo hayo alisema yamemsaidia sana katika kuhakikisha
kwamba kituo chake kinakuwa bora na kinachovutia watangazaji.
Alisema mafunzo hayo yamewafanya wajitambue kwani yamefanyika mfululizo kwa mara 5 na kuwafanya wabadilike.
Aidha
Meneja wa kituo cha Redio Jamii FADECO ya wilayani Karagwe, Adelina
Lweramula alisema kwamba anashukuru mafunzo kwa kuwa yamewafanya kuondoa
mawazo vichwani na kuweka mipango kazi katika karatasi na kuwezesha
wafanyakazi nao kufuatilia.

No comments:
Post a Comment