![]() |
| Waziri wa Ujenzi, Dk. Maguful |
VITENDO vya madereva na abiria
kupigwa, kuporwa, kutolewa lugha za matusi na wapiga debe katika kituo cha
mabasi Mbezi vimekuwa jambo la kawaida.
Kituo hicho kinasimamiwa na
Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), wakati Waziri wa Ujenzi Dk. John
Magufuli alipokizindua alipga marufuku kuonekana wapiga debe, wauza magazeti na
bodaboda ndani ya kituo hicho.
Hata hivyo agizo hilo, la
Waziri Dk. Magufuli, limepuuzwa na wapiga debe hao, ambao wamekigeuza kuwa mali
yao kwa kukiendesha wanavyotaka huku mamlaka ambazo zingeweza kuwadhibiti
zikifumbia macho vitendo hivyo vya kihuni.
Wakati Dk. Magufuli akitoa
agizo hilo, juzi usiku (saa 2:00), mwandishi ilishuhudia genge la wapiga debe
wakilivamia gari la kifamilia T 445 CKM lililokwenda kituoni hapo kwa ajili ya
kupokea ndugu zao waliokuwa wakitokea mikoani, wakidai wapewe sh 700 ambazo
wameziita kwa ni za kitengo.
“Huu ni utaratibu wa kituo
hiki kwa kila anayeingiza gari hapa lazima alipe unashangaa sh.700 mbona wapo
wenzako wanalipa sh 500, 1000 na 200 sasa kwa vile ya kwako ni gari ndogo
lazima uilipe hiyo tuliyokwambia,”alisikika mmoja wapigadebe hao.
Hata hivyo, mmiliki wa gari
hilo ambaye jina lake halikupatikana alipinga kutoa fedha, hizo jambo
lililowafanya wapigadebe hao waanze kuishambulia familia huku wengine
wakijaribu kuwaibia lakini walishindwa.
Wapigadebe hao
walitawanyika katika eneo hilo baada ya abiria waliokuwepo kituoni hapo
kusanyika katika tukio hilo.
Mwandishi aliwashuhudia
baadhi ya abiria wakiishauri familia hiyo kwenda kutoa taarifa polisi lakini
ilikataa ikidai kuwa kila mmoja kati yenu ameona maonevu hayo, hivyo
wanamuachia mungu ataamua.
Kati ya abiria
aliyeshuhudia tukio hilo, alikuwa Khamis Jongo, ambaye alisema matukio ya
kupigwa madereva na abiria katika kituo hicho yamekuwa yakijitokeza karibu kila
siku lakini hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi ya wapigadebe hao ambao wengi ni
watumiaji wa dawa za kulevya.
Alisema kuna kipindi
walimpiga dereva ambaye hakuvumilia, alikwenda polisi ambapo ilijaribu
kuwadhibiti kwa muda lakini hivi sasa wamerudi tena na kwamba wamekuwa
wakifanya vitendo hivyo bila kificho jambo linalowashangaza madereva na abiria
wanaotumia kituo hicho.
Hamisa Omari, alisema kuwa
anawaomba polisi wa kituo cha Mbezi kuwaondoa kituoni hapo wapiga debe hao
ambao wamekuwa kero katika kuwanyanyasa wanawake pindi wanapochagua gari la
kupanda.
Alisema serikali inapaswa
kuwa makini na wapigadebe kwani ni watu ambao wanachangia kwa kiasi kikubwa
kuliibia taifa kupitia fedha hizo wanazonyang’anya madereva kwani hazilipiwi
kodi na kwamba wako katika kila kituo nchini.

No comments:
Post a Comment