KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Thursday, 16 April 2015

WATANZANIA WAJIANDAA KUPIGA KURA YA KATIBA INAYOPENDEKEZWA

Na MatukiodaimaBlog

WAKATI 
watanzania wakijiandaa kushiriki  kupiga kura yao juu ya katiba 
inayopendekezwa  wananchi  wa kata ya  Nsalala  wilaya ya  Mbeya 
vijijini  mkoani Mbeya  wamedaia  kuwa idadi ndogo ya nakala  za katiba 
zilizopelekwa   katika kata  hiyo  wamekuwa  wakilazimika kukusanyika
vikundi vya  watu  watano hadi  kumi  ili  kusoma katiba   hiyo ama 
kuanzimana .
 
Wakizungumza na  timu ya  wanahabari  wa mtandao  wa  jinsia  Tanzania  (TGNP), 
waliofika  katika kata  hiyo kufuatilia  uelewa  wa  wananchi 
juu ya katiba   hiyo  inayopendekezwa wakazi  wa kata  hiyo  ya Nsalala   walisema  baadhi yao  bado mzunguko  wa  kufikiwa na nakala
ya  katiba chache  zilizotolewa katika  kata  hiyo  bado haujawafikia hivyo  hawajasoma chochote.
 
Bw 
Henson Mponi mkazi  wa  kijiji  cha  Nsalala  kata  ya Nsalala  wilaya 
ya  Mbeya  vijijini  alisema   kuwa  ni vema  serikali kuangalia 
uwezekano  wa  kusambaza  zaidi  vijijini  nakala  za katiba   hiyo 
ili  wananchi   weweze  kuzisoma  na  kuzielewa na  kuwa haoni  uharaka
wa  kukimbiza  zoezi hilo huku  wananchi wakiwa  gizani .
 
Alisema 
kuwa bunge la katiba  limemaliza kazi yake  ya  kuandaa katiba   hiyo 
hivyo  ni zamu ya  wananchi nao  kupewa  muda  wa kuipitia  na
kuielewa  kabla ya  kupita  kura  kwa  jambo  ambalo wao  hawalitambui.
 
Kwani 
alisema hadi  sasa   kijiji  chake cha Nsalala chenye   watu  701 
nakala  za katiba  ambazo walitangaziwa  kuwa  zimefika ni 36  huku 
kitongoji  cha  Nsalala   chenye watu  150 wamepewa  nakala  5  za 
katiba   hivyo shida  ya  kusoma  inatokana na  idadi  ndogo ya nakala
za  katiba  hizo  na  kupelekea  wananchi  kuanzimana  ama  kusoma kwa 
makundi makundi .
 
Alisema 
kuwa  wanachoshukuru  ni   kufikiwa mapema kwa katiba  hizo ambazo toka 
mwezi  wa  pili wananchi  walipewa katiba  hizo  ila  hadi  sasa bado 
mzunguko  wa  kufikiwa na  nakala  za katiba   hizo  ni mgumu  zaidi.

"Tunaomba  kuongezewa nakala  zaidi za katiba  kwani  vinginevyo 
shughuli za uzalishaji mali  kwa  wananchi  wakulima  hapa kijijini 
zitayumba  zaidi kutokana na  kusubiri kukusanyika  kusoma katiba 
hiyo…ushauri  wangu  ni  vema nakala  za katiba  zingeletwa kulingana 
na idadi ya  wananchi kama  tupo  150  basi nakala  150  zingeletwa  ili 
kila mmoja aweze  kuwa na nakala  yake na  kutenga  muda wake wa
kuisoma kuliko kusubiri kupokezana ama  kukusanyika makundi"
 
Hata 
hivyo alishauri  kama inawezekana  serikali kuzileta  katiba  nyingi 
zaidi na kuziuza kati ya Tsh 10,000 ama  20,000  ili  wananchi waweze
kununua wenyewe na  kujisomea  kuliko  hizo za  bure  ambazo hazitoshi 
kulingana na idadi ya  watu katika  kata  na vijiji  vya kata   hiyo.
 
Bw 
Aron Zambi  ni mjumbe  wa serikali ya  kijiji  cha Nsalala  alisema 
kuwa  hajafahamu  kuwa  serikali  imegawa  nakala   hizo  za katiba 
kwa  kuanglia uwiano  gani  kutokana na  kusambaza  idadi ndogo zaidi 
za nakala  za  katiba  hiyo .
 
Zambi 
alisema  kuwa  ni vema  wananchi  wakasoma  katiba   hiyo badala ya 
kutegemea  wana siasa  wawahamasishe  kuipigia  kura ama  kutoipigia 
kura  kwani  alisema  anachokiona  yeye  ni mwisho  wa  siku katiba 
hiyo  kupigiwa  kura ama  kutopigiwa kura ya  ndio kutokana na  wengi
wao  kutoisoma.
 
Kwani 
anasema  hata hatua ya  tume  ya Taifa  ya  uchaguzi (NEC)  kusogeza 
mbele zoezi la  kura  za maoni  bado halitasaidia  kwani kama  nakala 
za katiba  zaidi  hazitasogezwa kwa  wananchi hata kama  zoezi hilo
litasogezwa  hadi  mwakani kama  wananchi hawana nakala  za katiba 
mkononi uwezekano  wa  kuzitafuta  wenyewe  hautakuwepo hivyo ni  sawa 
na  bure.
 
Afisa 
tendaji  wa kijiji cha   Nsalala  Bw Lwitiko  Mwaidindi  alisema 
kuwa   alipokea  nakala 36  pekee za katiba  wakati kijiji hicho 
kinajumla ya  wananchi  wenye  umri wa  kupiga  kura 701 .
 
Afisa 
mtendaji  kata  ya Nsalala  Bw  Joseph Stima  alisema  kuwa  kata 
yake  inajumla ya  wapiga kura 19,346 wakiwemo wanaume ni 9143 na 
wanawake ni 10203 ila  idadi ya nakala  za katiba  inayopendekezwa 
waliyoipata  ni 261 pekee  na  kuwa nakala  hizo  zimesambazwa katika 
vijiji  vyote pamoja  na makundi  maalumu  kama wanawake ,walemavu,
taasisi  mbali  mbali  na  maeneo mengine  yenye mikusanyiko mbali 
mbali   pamoja na viongozi  wa  vitongoji  vyote   6 vya kata  hiyo 
ambavyo ni  Tunduma Road , Mshikamano,Mapinduzi , Ndola  na Nsalala
kulingana na  idadi ya watu katika vitongoji hivyo..

No comments:

Post a Comment