Mpaka sasa bado kuna watu ambao wameendelea kushikiliwa mateka katika hicho.
Serikali ya Kenya imemtaja Mohammed Kuno ambaye anajulikana kwa jina
la Gama Adhere kama mshukiwa aliyepanga shambulio hilo, ambalo
limegharimu mpaka sasa maisha ya watu 15.
Serikali ya Kenya imetoa zawadi nnono ya dola 53,000 kwa
atakayemkamata Mohammed Kuno au atakayetoa taarifa kuhusu mshukiwa huyo.
Wakati huohuo Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, ametuma risala za rambi
rambi kwa familia za watu waliouawa katika shambulio lililotokea katika
chuo kikuu cha Garissa mashariki mwa Kenya.Rais Uhuru Kenyatta pia
amewahakikishia raia wa Kenya kuwa serikali yake imechukua hatua ya
kuongeza vikosi vya usalama katika eneo hilo.
Rais Kenyatta amewatolea wito raia wa Kenya kuwa watulivu, wakati
vikosi vya usalama vikiendelea na operesheni ya kuwaska washambuliaji.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Kenya, shambulio hilo lilianza
saa za swala mapema asubuhi, kwenye majira ya saa kumi na moja na nusu
leo Alhamisi. Idadi ya watu walioendesha shambulio hilo haijajulikana
Kwa mujibu wa gazeti la Kenya la The Standard, wanafunzi waliofaulu kuondoka chuoni hapo, wamesema waliwaona watu watano wenye silaha.
Kwa mujibu wa polisi ya Kenya, watu hao wenye silaha, walianza kufyatua risase walipoingia chuoni hapo.
No comments:
Post a Comment