HOSPITALI maarufu kwa kutibu vigogo wa serikali,
African Medical Investment (AMI), hatimaye imefutwa rasmi baada ya jengo la
hospitali hiyo kukabidhiwa kwa mmiliki wa jengo hilo kwa nguvu ya mahakama.
Nao wafanyakazi wa hospitali hiyo wamesema
hawajui hatima yao, baada viongozi wao kuzima simu zao.
Hali hiyo ilitokana na mri ya Mahakama Kuu kuagiza
mali za hospitali hiyo zikamatwe na jengo la hospitali hilo lirejeshwe kwa
mmiliki wake kutokana na kushindwa kulipa kodi ya pango sh. bilioni 3.2 kwa
zaidi ya miezi 26.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es
Salaam le, Meneja Masoko wa Kampuni ya Madalali (MEM), Elieza Mbwambo,
alisema kazi yao ilikuwa ni kukamatama mali na kukabidhi jengo, masuala ya
kudai fedha ni jukumu la mmiliki.
Alisema kuwa walifikia hatua hiyo baada ya
uongozi wa hspitali hiyo kutii amri ya mahakama ya kuwaondoa wagonjwa wote na
kwamba mali walizokamata wataziuza.
“Wiki mbili zilizopita tulikuwa hapa kukamata
mali na tuliwapa taarifa wagonjwa wote waliokuwa hapa waondoke na leo
tunashukuru wagonjwa wote wameondoka na leo tunamkabidhi jengo mwenye
mali,”alisema Mbwambo.
Mbwambo, alisema vifaa vyote vilivyokamatwa
vitaviuzwa, hata hivyo, fursa itatolewa kwanza kwa mmiliki wa jengo hilo.
Akizungumza kwa niaba ya Kampuni ya Navtej Singh
ambao ndiyo wa jengo hilo, Zulfiqar Hassanali, alisema baada ya kukabidhiwa
jengo lao, wanatarajia kufungua hospitali kama mwanzo kwa vile eneo hilo la
Msasani halina huduma hiyo zaidi hapo.
“Bado hatujampata mtu kwa sababu baada ya
kutokea tukio hili kuna watu wengi wamejitokeza kuomba jengo hili kwa kuendesha
shughuli hizi,”alisema Hassanali.
Wafanyakazi
Msemaji wa Wafanyakazi, Roselin Sesoa, alisema
walishangazwa na hatua hiyo kwa vile ongozi uliendesha mgogoro kwa usiri mkubwa
ambao hawakuwa kuujua.
Alisema, kutokana na mazingira hayo, wanashindwa
kujua hatma ya haki zao kwamba watazipata wapi kwani uongozi wa hospitali hiyo
haupatikani na wala hawajui waliko kimbilia.
“Unajua tuko 100 ambao hatujui jinsi ya kupata
haki zetu kwani tangu kutokea kwa tukio hili viongozi hawajulikani waliko
tukiwapigia simu hazipokelewi na hawa ni wageni,”alisema Sesoa.
Sesoa, aliitaka serikali kuwa makini katika
kutoa fursa za uwekezaji kwa wageni kwani kama hawa wangekuwa wenyeji naamini serikali
ingeweza kuwafuatilia kirahisi katika kusaidia wapate haki zao.
No comments:
Post a Comment