KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za
Serikali (PAC), imeuagiza uongozi wa Mkoa wa Mara kuharakisha ujenzi wa nyumba
ya Mkuu wa Wilaya ya Serengeti ili kukomesha matumizi mabaya ya fedha za serikali
kwa kumlipia kodi ya kuishi hotelini.
Mkuu huyo wa wilaya ameishi hotelini kwa
zaidi ya miezi miwili tangu alipoteuliwa na kwamba hadi sasa ametumia zaidi ya
sh. milioni 600.
Akizungumza juzi jijini wakati wa
kujadili taarifa za mkoa huo wa Mara, Kaimu Mwenyekiti wa Kamati, hiyo, Aden
Rage, alisema kitendo cha kumuacha mkuu huyo wa wilaya kuendelea kuishi hotelini
hakileti picha nzuri.
Alisema kutokana na kamati hiyo
kutoridhishwa na taarifa hiyo ambayo ilikuwa ikionesha kilichobaki katika
ujenzi wa nyumba hiyo ni tenki la maji ni vema mkoa huo ukakamilisha kazi hiyo
mara moja.
Rage, alisema kuwa kamati hiyo
inauagiza ungozi wa mkoa huo kamilsha kazi hiyo na kufikisha nakala katika
ofisi ya CAG, Ofisi ya Bunge na kamati yenyewe.
Kamati hiyo iliutaka uongozi wa Mkoa wa
Mara kutumia utaratibu na sheria sahihi wa manunuzi ya serikali ili kuepusha
wizi na ubabaishaji unaoweza kutokea.
Katika hatua nyingine Kamati hiyo haikuridhishwa
na taarifa za utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2014/2015, kutokana na
kuwa na mapungufu mengiAkizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Bunge
jijini Dar Salaam mara baada ya kumaliza vikao vya wiki mbili za kupitia
taarifa hizo, Rage alisema kwamba katika kuzikagua hesabu za mikoa yote zilibainika
kuwa na hati za mashaka.
“Mikoa yote ina hati za mashaka kwa
sababu katika kukagua taarifa zao, mara utaona milioni kadhaa zimeliwa bila
maelezo ama milioni kadhaa zimeingizwa katika matumizi yasiyokuwa yake au
hakuna nyaraka za matumizi huiska” alisema Rage
Alitoa mfano wa mikoa miwili wa Mara na
Tanga ambayo walikuwa wakiijadili kwa siku ya jana kama
hitimishwa kwamba nayo imefanya vibaya katika taarifa yake .
Kauli ya wabunge wa kamati hiyo
imetokana na manunuzi feki katika vitu mbalimbali yaliyofanywa katika Hospitali
ya Mawezi ambapo fedha zaidi ya mil 20 za kununulia mashine ya kufulia zimeliwa bila kufanyia kazi iliyopangwa
pamoja na kununua dawa nje ya Bohari Kuu ya Dawa (MSD).
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Hery
Ally Khamis alisema juzi kuwa licha ya kutakiwa kufuata utaratibu huo pia
watekeleze maagizo waliyokwisha yatoa katika kipindi cha mwaka 2012 ikiwa ni
pamoja na aliyetapeli fedha za kununulia mashine ya kufulia katika hospitali ya
Mawenzi kuzirudisha.
Wakichangia hoja hiyo Mjumbe wa kamati
hiyo Ismail Aden Rage alisema kuwa uongozi wa
mkoa ulitaka hapo awali suala hilo
lisikilizwe nje ya mahakama na kukubaliana kulipwa kwa fedha hizo lakini hadi
leo kati ya mil 20 imelipwa mil 3 tu jambo ambalo ni ubabaishaji.
Naye Mjumbe Ally Kessy alisema
aliyetakiwa kulipa mil 20 ilikuwa kwa miaka mingi iliyopita hivyo akashauri
akianza kulipa aweke na riba.
Hata hivyo Mjumbe ambaye ni Mbunge wa
Kibiti Abdul Malobwa alishangazwa na bajeti ya Mkoa wa Kilimanjaro kupatiwa
fedha nyingi za bajeti hadi na ziada na kurudishwa hazina huku mikoa mingine
ikiwa haina fedha za kutosha.
Katika hilo
RAS hakuwa na majibu na kutakiwa atakaporudi tena kutoa majibu huku wabunge hao
wakihoji kama kuna mtu hazina anawaunganishia
na kupata kiasi hiko kikubwa cha fedha.
Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa
Kilimanjaro, (RAS) Severine Kahitwa alizungumzia utapeli wa mil 20 na kusema
kuwa walipogundua kuwa ni tapeli waliamua kumpeleka mahakamani na walipoona kuwa hawakufanya sahihi
walishauriana nje ya mahakama na mtu huyo kuanza kulipa fedha hizo.
Hata hivyo alisema tayari wameanza
kujirekebisha na kufuata utaratibu wa manunuzi kama
serikali inavyoagiza sambamba na kumfuatilia aliyechukua mil 20 kurudisha kwa
wakati.
wisho
No comments:
Post a Comment