Mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe akiwhutubia wakazi wa kijiji cha Mavanga wilayani Ludewa muda mfupi baada ya kukabidhi msaada wa vitu mbali mbali vya ujenzi vyenye thamani ya Tsh milioni 40 katika kijiji hicho
Na MatukiodaimaBlog
MBUNGE
wa jimbo la Ludewa mkoani Njombe Deo Filikunjombe amesema baadhi ya
wabunge, mawaziri na watendaji wabovu serikalini wanakichafua chama cha
mapinduzi ( CCM ).
Filikunjombe, alisema kuwa
CCM ni chama makini na kinachopendwa ila shida ipo kwa baadhi ya
watu waliopo ndani ya CCM na serikali ambayo ni bomu.
Mbunge
huyo alitoa kauli hiyo leo katika kijiji cha Mavanga wakati akijibu
maswali ya wananchi na viongozi wa Vyama vinavyounda Katiba ya Wananchi (
Ukawa), kuhusiana na CCM kuwateulia wananchi viongozi wasio na sifa
kugombea nafasi mbali mbali.
Alisema, kama kila
mmoja angetimiza wajibu wake katika nafasi yake hakuna mpinzani ambae
angechaguliwa ila kuchaguliwa kwa wapinzani ni kushindwa kwa wale
waliowaamini kutoka CCM kushindwa kuwajibika kwa wananchi waliowaamini.
Filikunjombe,
alisema atakuwa mbunge wa mwisho kunyoshewa kidole na watanzania
wakiwemo wananchi wake wa Ludewa kwa kushindwa kuwatumikia wananchi na
chama chake cha CCM .
Alisema, hakuomba ubunge kwa ajili ya kujinufaisha binafsi ila aliamua
kugombea ili kuwatumikia wana Ludewa kwa kuwapelekea maendeleo hivyo k
azi yake kwa sasa hadi mwisho wa ubunge wake ni kuleta maendeleo kwa
wananchi wake na kuona ahadi zake zinatimia kwa muda uliopangwa na si
kujinufaisha kwa wakati.
"Naomba kwanza mtambue kuwa wabunge wote tulipo fika bungeni kwa mara ya
kwanza tulikopeshwa sh. milioni 90 kwa ajili ya kununua gari la
kutembelea na Mimi kwa kuwa nilikuwa na gari pesa hizo niliamua kununua
gari la wagonjwa Mlangali ambao hawakuwa na gari la wagonjwa
….lengo langu kutumikia wananchi na kuwatatulia kero zao si
vinginevyo”alisema
Akielezea msaada huo wa vitu mbali
mbali vyenye thamani ya Tsh milioni 40 alivyotoa alisema ni pamoja na
kitanda cha kujifungulia wajawazito chenye thamani ya Tsh milioni
5.2, Darubini, pesa ya taslimu sh. milioni 1 bati zaidi ya 500, rangi
debe 20, saruji mifuko 525 na vifaa vingine vingi kwa ajili ya
kuchangia ujenzi wa miradi mbali mbali ya kijiji na ujenzi wa
makanisa, shule na wodi ya wazazi.
Awali
viongozi ukawa wa kijiji cha Mavanga kata ya Mavanga walimpongeza
mbunge huyo kwa kuwa mbunge wa mfano Ludewa japo wapo viongozi
wengi ndani ya chama chake ni wabovu.
Mwenyekiti
wa Ukawa Mavanga John Mligo akishukuru kwa msaada huo wa vifaa na
fedha toka kwa mbunge Filikunjombe alisema kama wabunge na viongozi wote
wangefanya kama mbunge huyo kamwe wananchi wasingekichukia chama
hicho.
Akizungumza
katika mkutano huo mwenyekiti huyo wa Ukawa na mwenyekiti wa serikali
ya Kijiji cha Mavanga Hilmar Mpambichaka (Chadema), walisema wao
kama viongozi wa upinzani hawana shaka na uwakilishi wa mbunge
Filikunjombe ndani ya jimbo hilo na nje ya jimbo hilo.
"Tumekuwa na wabunge saba ambao wametangulia kabla ya Filikunjombe ila
uwakilishi wake umekuwa wa kuigwa na wabunge wengine na kama wabunge
kote nchini wangekuwa watendaji hivyo huenda upinzani nchini
usingekuwepo,”alisema Mligo
alisema chanzo cha kijiji hicho kuchagua mwenyekiti wa Serikali ya
kijiji kutoka Chadema ni baada ya viongozi wa CCM kuonyesha kuwa mbali
na wananchi na baadhi yao kutafuna fedha za michango ya wananchi.
Mligo alisema shida ndani ya CCM ni vita ya wenyewe kwa wenyewe ndio
ambayo imekuwa ikiwachanganya wananchi na kujikuta wananchi wanaingia
katika
mgawanyiko na kuchagua wapinzani.
Alisema
wakati wa kampeni hata wasio na sifa wanataka kuchaguliwa kwa kutumia
rushwa, hivyo kutaka kwa Ludewa kutambua wazi mbunge anayekubalika ni
Filikunjombe pekee na kuwa hawahitaji mtu zaidi ya mbunge wao
aliyewavusha na kuwafikisha katika maendeleo ya kweli.
Huku
mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Mpambichaka akiwataka
wananchi wa Ludewa kuacha kuonja sumu kwa kubadili wabunge na kuwa
utendaji wa Filikunjombe hakuna wa kumfananisha nae.
Alisema
kuwa wamepata kushuhudia utendaji wake ndani ya bunge kupitia kamati ya
PAC kwa kupambana na ufisadi kupitia Escrow na kuwafanya mawaziri zaidi
ya watatu kujiuzulu.
Pia
kupitia utendaji wake ndani ya jimbo amefanikiwa kuwavuta wana Ludewa
ambao siku zote walikuwa wakiona aibu kuweka wazi kuwa ni wakazi wa
Ludewa na badala Yake kudanganya kuwa wao ni wazaliwa wa Mkoa wa Ruvuma
kutokana na awali
Ludewa kuwa nyuma kwa maendeleo.
"Toka Filikunjombe ameingia madarakani mwaka 2010 na kuwepo kwa kasi ya
maendeleo ndio tunashuhudia wana Ludewa wakirejea Nyumbani na
kujitangaza kuwa wao ni wakazi wa Ludewa tofauti na zamani wengi
walikuwa wakijificha kwa aibu,"
Hata
hivyo alisema wapo wabunge ambao wamekaa majimboni muda mwingi kama
akina Mzindakaya huko Sumbawanga ila siku zote ni mtu wa kueleza jinsi
alivyofanya Kazi na Mwl Julius Nyerere ila si kujipambanua namna gani
alivyoleta maendeleo jimboni
Kuhusu
misaada mbali mbali iliyotolewa na mbunge huyo kijijini hapo mwenyekiti
huyo alisema kwa mara ya kwanza toka wabunge 7 waliopita kijiji hicho
kimepata kupata misaada mingi kutoka kwa mbunge huyo.
|
No comments:
Post a Comment