![]() |
| Mwenyekiti wa Tume, Lubuva |
TUME ya Taifa ya Uchaguzi
(NEC), inatarajia kugawa majimbo ikiwa ni maandalizi ya uchaguzi mkuu
unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Tume ya uchagu ndiyo yenye
jukumu la kuchunguza mipaka na kuigawa Jamhuri ya Muungano katika maeneo mbalimbali
kwa ajili ya uchaguzi wa Wabunge kwa mujibu wa Ibara ya 74(6) (c) ya Katiba ya Tanzania
ya waka 1977.
Hata hivyo Tume hiyo
haikutoa idadi ya majimbo kwa kuwa inategeme kupokea maombi kutoka hatika
Halmashauri na kwamba kesho itatoa tangazo kwenye gazeti la serikali na kueleza
kila kitu.
Akisoma taarifa kuhusu
ugawaji wa majimbo hayo mbele ya viongozi wa vyama vya siasa nchi, jijini Dar
es Salaam jana, Kurugenzi wa NEC, Julius Malaba, alisema kwa kuwa huu ni mwaka
wa uchaguzi, hivyo tume inatakiwa kuanza maandalizi mapema ili kuweza
kufanikisha uchaguzi huo.
Alisema, moja ya maandalizi
ambayo yanatakiwa kufanywa na tume hiyo ni kuchunguza mipaka na kugawa majimbo
kwa sababu kuna halmashauri mpya zimeanzishwa, na kwa mujibu wa Sensa
iliyofanyika 2012, idadi ya watu imeongezeka.
Malaba, alisema katika
ugawaji huo tume itakuwa na vigezo maalumu huku ikizingatia mipaka ya
kiutawala.
Alisema kwanza mgawanyo huo
utazinga wastani wa idadi ya watu katika jimbo inayopatikana kwa kuchukua idadi
ya watu wote nchi nzima na kuwagawanywa kwa idadi ya majimbo yaliyopo.
‘Population quota’
itazingatia hali halisi ya idadi ya watu mijini na vijijini.
“Kigezo cha ‘Population
quota’ ndicho kigezo kikuu na cha kwanza kitakachotumika katika kuamua majimbo
gani yagawanywe,”alisema Malaba.
Kwa mujibu wa makadirio ya
Ofisi ya Takwimu mpaka 2015 Watanzania wote kwa upande wa Bara watakuwa
wamefikia milioni 47, 110,506.
Kwa upande wa majimbo ya
mijini watu milioni 10,069,159 na vijijini ni 37,041,347, hivyo ‘population
quota’ kwa upande wa majimbo ya mijini itakuwa ni 325,000 na kwa upande wa
majimbo ya vijijini itakuwa ni 235,000.
Alisema kwa maana hiyo,
majimbo yatakayostahili kuwasilisha maombi kwa mujibu wa utaratibu ulioanishwa
ni yale tu yenye idadi ya watu zaidi ya idadi ya ‘population quota’.
Idadi ya watu itakayotumika
ni ile iliyotokana na makisio ya ongezeko la watu hadi Julai, 2015 kwa mujibu
wa sensa ya mwaka 2012.
Majimbo yenye watu wengi
yatafikiriwa kugawanywa.
Malaba alisema takwimu
zitakazotumika katika kigezo hiki zitapatikana katika Ofisi ya Taifa ya Takwimu
(NBS).
Upatikanaji wa mawasiliano
hapa itaangaliwa urahisi wa mwakilishi kuwafikia/kuwasiliana na anaowawakilisha
katika maana ya barabara, simu, vyombo vya habari.
Hali ya kijiogrfia,
itangalia jimbo liko sehemu gani kwa mfano , maeneo ya mlimani, visiwani au
mabondeni kwa lengo la kuona ni kwa jinsi gani litawasilishwa kwa ufanisi.
Alisema kigezo kingine
kitakuwa ni uchumi hapa uangalifu utachukuliwa, ili maeneo ambayo yako juu
kiuchumi yasimeze kiuwakilishi maeneo yaliyo chini kiuchumi, maeneo yalio chini
kiuchumi yatafikiria.
Aliongeza kuwa ukubwa wa
eneo la jimbo pia utaangaliwa na maeneo yenye maeneo makubwa yatafikiriwa.
Kingine ni mipaka ya
kiutawala ambapo katika kugawa majimbo tume itazingatia mipaka ya kuitawala.
Malaba, alisema pale ambapo
mipaka ya utawala itabadilika kabla ya tume kufanya ugawaji wa majimbo, tume
itazingatia mabadiliko hayo.
Aidha, alisema jimbo moja
lisiwe ndani ya wilaya/halmashauri mbili, kigezo hiki kitazingatiwa ili
kuepusha mwakilishi kutumikia wilaya/halmashauri mbili tofauti kwa wakati
mmoja.
Alisema pia Kata moja isiwe
ndani ya majimbo mawili na mpangilio wa maeneo ya makazi ya watu yaliyopo.
Malaba alisema ugawaji huo
pia utazingatia mazingira ya Muungano, kama inavyoeleweka kuwa Tanzania ni
nchi ya inayounganisha nchi mbili, kwa hiyo ugawaji wa majimbo utazingatia pia
upekee wa mazingira ya Muungano.
Alisema tume itazingatia
Uwezo wa Ukumbi wa Bunge, katika kugawa majimbo ni muhimu kwa tume kuzingatia uwezo
wa ukumbi wa Bunge ili kuepuka kuzidisha idadi ya wabunge kupita nafasi iliyoko
katika ukumbi huo.

No comments:
Post a Comment