KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday, 7 June 2015

CCBRT YAFUNGUA KIWANJA CHA MICHEZO YA WATOTO

HOSPITALI ya CCBRT iliopo Msasani wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam imefungua kiwanja cha michezo tofauti tofauti  ya watoto hospitalini hapo. 
Akizungumza  wakati wa  uzinduzi wa kiwanja hicho  hivi  karibuni, Mwenyekiti   wa kamati ya  mashindano ya  mbio za mbuzi ‘Dar es Salaam  Charity  Goat Races’, Karen Stanley  alisema  kitasaidia katika kuhamasisha afya ya watoto walioko wodini  kwa kucheza,kupumzika na kuweza kujumuika na watoto wengine. 
Alisema kuwa kuwa CCBRT ilitambua kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kuboresha kiwanja cha michezo cha watoto kilichokuwa kimechakaa kwa kujenga upya na kuongeza ubora wa kivuli cha kupumzika. 
Stanley, alisema michezo ina sehemu kubwa katika ratiba za matibabu  ya watoto waliopo hospitalini haswa walioko kwa muda mrefu kwa lengo la kuwaondolea mawazo na kuwafanya wawe sehemu ya jamii iliyona afya bora.
“Kulazwa hospitalini si tukio la kawaida na mara nyingi husababisha msongo kwa watoto na familia zao, hivyo kwa kufunguliwa kwa kiwanja hiki kitawajenga watoto kisaikolojia." Alisema na kuongeza kuwa 
“Kuwepo kwa eneo hili ambalo watoto wanaweza kucheza,pia husaidia kuwapa muonekano mzuri juu ya muda wao  kwa muda wote watakaokuwa hapa hospitalini”  
Alisema kwa kupata uwanja huo utawafanya watoto kuweza kumudu baadhi ya matibabu yakiwemo ya upasuaji na magonjwa mengine wakati wakiwa  hospitalini. 
Stanley, alisema kuwa uwanja huo ulianza kujengwa Desemba mwaka jana na kukamilika rasmi mwezi juni mwaka huu kwa  udhamini wa mashirika manne ya Irish Aid, Dar es Salaam Goat Races, Corona Society of Tanzania na Familia ya Wetzel.

No comments:

Post a Comment