BAADHI ya wakazi wa jiji la
Dar es Salaam, wameutaka Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kuwapa nafasi ya makada wake
wanaotaka kutangaza nia ya kuomba uteuzi wa kuwania nafasi ya urais kupitia
umoja huo ili wananchi wawatambue mapema.
Walisema hivyo, kwa vile
wanaamini kuwa utaratibu huo ambao unafanyika ndani ya Chama Cha Mapinduzi
(CCM), unaonesha kuwa ni wa kidemokrasia na unazingatia matakwa ya kila
mwanachama.
Wakizungumza kwa nyakati
tofauti jijini Dar es Salaam leo, walisema kukaa kumya kwa umoja huo
kunawajengea wasiwasi baadhi ya wanachama kwamba huenda umoja huo umeshindwa
kufikia muafaka katika malengo yao.
Mohamed Gema, Mkazi wa
Manzese, alisema baada ya watia nia wa CCM kujitokeza imewasaidia kujua ukweli
wa kila mmoja katika kuzitambua kero za wananchi na uwezo wao wa kuzitatua uko
uje.
“Kiukweli inaonekana wote
wanazitambua kero zinazowakabili wananchi lakini hawaoneshi mikakati ya
kuzimaliza pindi watakapoingia madarakani,”alisema Gema.
Alisema kutokana na
mazingira hayo wanaamini kuna ulazima wa kuwajua watia wa umoja huo ili
wananchi wa wajue nao wanazijuaje kero za wananchi na kwamba wanamikakati gani
ambayo itasaidia kuwakomboa wananchi katika lindi la umasikini.
“Nchi hii inataka kiongozi
amabye anazitambua kero za na agenda za wananchi na sio watu ambao ukiwaangalia
tu sura zao hazioneshi kabisa kuguswa na matatizo ya wananchi bali wanalenga
masilahi yao pindi watakapoingia Ikulu,”alisema Gema.
Estera Bwire, alisema
wanautaka Ukawa kufanya hivyo haraka kwani wamechoshwa kutaniwa na watani zao kuwa
hawana mgombea na kwamba wanasubiri makapi kutoka CCM.
Alisema utaratibu wa
kuwapata wagombea katika Ukawa hauna tofauti na ule wa CCM hivyo ingekuwa ni
vema wakajitokeza tukawajua wanaotaka urais kwa ajili ya kuwapima uwezo wao.
“Wagombea wajitokeze na
baadae wakae kwenye vikao vya ngazi ya juu kwa ajili ya kumteua mmoja ambaye
atakuwa chaguo la umoja huo, ambaye atapambana na yule wa CCM na vyama vingine,”alisema
Ester.
No comments:
Post a Comment