KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Monday, 1 June 2015

WASIRA: IKULU NI SEHEMU TAKATIFU NA SI KIJIWE CHA WALA RUSHWA


WAZIRI wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wassira amewaeleza Watanzania kuwa wawe makini na baadhi ya viongozi wala rushwa wanaotaka urais, kuigeuza Ikulu kama kijiwe cha walashwa.

Wassira, aliyasema hayo jana wakati akitangaza nia ya kuomba ridhaa ya kugombea urais wa awamu ya tano kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika ukumbi wa B.o.T ulioko jijini Mwanza.
Alisema amekuwa kiongozi katika awamu zote lakini hajawahi kuwa na kashfa ya wizi akitolea mfano wizi wa EPA na Tegeta Escrow ambapo zote hizo jina lake halikutajwa kwamba hakuhusika.
Wasira, alisema kama Ikulu atawekwa kiongozi mpenda rushwa, kunauwezekano, kiongozi huyo akweza kuja kuuza mipaka nchi.
“Mimi sio mwizi kama ningekuwa mwizi ningeweza kuwaiba hata mbolea yenu pale Wizarani,”alisema Wasira.

Wasira, alisema kuna baadhi ya watu wamekuwa wakiizungumzia rushwa fasheni wakati hakuna wa kupinga kuhusu tatizo hilo ambalo limekuwa hadi kuifanya ikose maendeleo.
“Mimi sio mla rushwa na kuna baadhi ya watu mkiwaona wananozungumzia tatizo rushwa hebu jaribuni kuwapima kama kweli inawakera, kwani kuna wengine walizungumzia tatizo la rushwa kama fasheni lakini haliwaumizi.
“Mwalimu Nyerere aliwahi kusema, mtu anayekerwa na rushwa akizungumzia tatizo la rushwa muangalieni machoni…nimeitumikia Tanzania katika awamu zote lakini kwenye kashfa ya EPA sikutajwa na hata ya Esrow sikutajwa pia, na sio kama siwezi kuiba, ningeiba hata mbolea zenu kwasababu najiamini.
Mwalimu Nyerere alishawahi kuniambia, Wassira unahitaji uongozi au utajiri? Kama unataka utajiri nenda kafanye biashara. Kama umepata baada ya kuwa Waziri basi moja kwa moja wewe utakuwa ni mwizi, kwasababu mshahara wa mwisho wa mwezi hauwezi kukutajirisha, biashara hauna halafu unatajirika huu ni wizi.
“…alisema mtu kama huyu aogopewe kama ukoma, hivyo Ikulu hatuwezi kuweka mla rushwa, mkiweka mla rushwa siku nyingine atauza Ikulu yenu,” alisema Wassira.
Akielezea vipaumbele vyake endapo atachaguliwa kuwa rais, alisema atahakikisha kuwa naimarisha bandari ya Tanga na Dar es Salaam pamoja na kutengeneza barabara ikiwemo ile ya kutoka Dar es Salaam hadi Chalinze.
“Awamu ya nne imefanya mambo makubwa vizuri katika suala la kutengeneza barabara, zilizobaki zitatengenezwa, tutashirikiana na sekta binafsi katika kujenga kutoka Tanzania mpaka Kigali na kwasasa tunampango wa kuanza kutengeneza barabara kutoka Dar es Salaam  hadi  Chalinze na badala ya hapo tutaendelea na nyingine,” alisema Wassira.
Wasira, alisema katika rasilimali za taifa, serikali lazima ichukue hatua, katika kuwasaidia wachimbaji wadogo ili waweze kuondokana na migogoro na pia zisaidie kupambana na umaskini na zitumike kwa faida ya kila mmoja.
Alipoulizwa swali na mwandishi wa habari wa Raia Mwema kuhusu wizi uliopo serikalini na ripoti mbaya za Mkaguzi na Mdhibiti wa hesabu za Serikali (CAG), Wasira alisema ufike wakati mkaguzi huyo apewe madaraka kisheria kwamba anatakapowabaini wezi haina haja ya kufikish ripoti kwa rais, bali aagize wakamatwe na kufikishwa mahakamani.

Alisema atahakikisha kuwa atakapokuwa rais mambo hayo yanasafishwa kabisa na hakuna atakayesamehewa katika hilo.

No comments:

Post a Comment