![]() |
| Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kinondoni, Mussa Natty |
Akizungumza
na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Natty, alisema kwa vile suala hilo ndio amelipokea
hivyo hawezi kulitolea majibu ya haraka.
Alisema,
anatarajia kufanya hivyo baada ya kukutana, watendaji hao, kupata taarifa kisha
kuzifanyia uchunguzi kwa ajili ya kubaini kama
kweli wapo waliofanya makosa hayo ndipo wachukuliwe hatua za kisheria.“Taarifa
hii naichukua kama vile nimepewa na raia na
msamalia mwema na kwa kuwa ni wajibu wangu nitaifanyia kazi haraka, nikikata
simu tu namuita Mtendaji, aje hapa alete taarifa kuhusu madai hayo,”alisema
Natty.Naye
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa huo, Jonas Halimoja, alisema mfanyabiashara huyo
hatambuliki katika ofisi ya mtaa kwa sababu eneo alilojenga halina vibali vya
mtaa ikiwemo fomu maalum ambayo ingemuwezesha kupata leseni ya makazi.“Mimi
na wakazi wa mtaa huu tumeshangaa kumuona mfanyabiashara huyu akivamia barabara
hii pamoja kuziba, mitaro ya maji, kufunika mabomba ya Mamlaka ya Majisafi na
Majitaka (Dawasco), tena huku akiwa hana leseni ya makazi ya mtaa huo jambo
ambalo limenishtua,”alisema Halimoja. Awali wakazi wa Mtaa huo, kwa nyakati tofauti walisema tangu kuzibwa kwa barabara hiyo kumewasabishia kero kubwa ikiwa ni pamoja na kukwama shughuli zote za kijamii katika mtaa huo.“Hatuwezi kuingiza magari kwa ajili ya kuja kubeba maiti kwenda kuzika, wagonjwa kwenda hospitali na kibaya zaidi mvua zilizopita tulitaabika kwa mafuriko kutokana na kuzibwa mitaro huu ni unyanyasaji,”alisekika mmoja wakazi hao.Walisema pamoja na mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo kuwasihi kuwa wavute subira wakati mgogoro huo unashughulikiwa, wanaamini kuwa iko siku wataubomoa kwa nguvu.Aidha, walisema ili wasifikie hatua hiyo wanamuomba Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi Williamu Lukuvi, atambue kilio chao hicho.

No comments:
Post a Comment