![]() |
| Dk. Magufuli |
KITENDO
cha Shirikisho la Soka Tanzania(TFF), kumtangaza mgombea urais wa CCM, Dk. John
Magufuli kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Kombe la Kagame, kimezidi kuibua
hisia tofauti miongoni mwa wadau katika jamii.
Wengi
wao wanahoji mantiki ya Rais wa Shirikisho hilo, Jamal Malinzi, kufanya hivyo
katika kipindi hiki ambacho vyama vya siasa vipo katika mchakato wa kupata
wagombea wao katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Chama Cha Kijamii (CCK), Renatus Muhabhi, alisema
uamuzi wa Malinzi na TFF yake si sahihi, kwani ni sawa na kuanza kumpigia debe.
Alisema
kwa mazingira yalivyo, Dk. Magufuli ataitumia nafasi hiyo kuanza kujipigia debe
na chama chake, jambo ambalo si haki, kwani wengine bado hawajapata fursa hiyo.
“Dk.
Magufuli hafahamiki kimataifa, hivyo anatengenezewa mazingira
ya
kuanza kujinadi kupitia michuano ya Cecafa inayoshirikisha nchi za ukanda wa
Afrika Mashariki na Kati,” alisema.
Muhabhi,
alisema hivi sasa kuna upotoshaji mkubwa unaofanywa na CCM wa kuwaaminisha
wananchi kuwa, mgombea huyo kama vile tayari ni rais, wakati bado ni mgombea
sawa na wa vyama vingine.
“Niwaombe
wananchi wakipuuze chama hicho cha CCM kwa kumfanya mteule huyo kama tayari ni
rais, tunapinga kumpa ulinzi kama Rais wa nchi, pia tunataka wakati wa kampeni
ndipo wapewe ulinzi,” alisema.
Muhabhi,
ametoa wito kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kuwazuia wagombea waliothibitishwa
na vyama vyao na tume hiyo kujinadi
kabla ya
kipindi maalumu cha kampeni.
Juzi TFF
kupitia kwa Ofisa Habari wake, Baraka Kizuguto, ilimtangaza Dk. Magufuli kuwa
mgeni rasmi katika ufunguzi wa michuano hiyo na kuibua mikanganyiko na hisia za
kisiasa miongoni mwa wadau wa michezo, wakihusisha na kampeni za kisiasa kwenda
kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba.
Aidha,
baadhi ya wadau hao walielezea TFF kujiingiza kwenye kampeni za kisiasa
kutaathiri maendeleo ya mchezo huo hapa nchini.

No comments:
Post a Comment