KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Thursday, 16 July 2015

WANAVYUO WAHAMIA (TIMU LOWASSA), CHADEMA



BAADHI ya Wanavyuo wanomuunga mkono Mbunge wa Monduli Edward Lowassa (Timu Lowassa), wamejiunga  na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), baada ya kutoridhishwa na mchakato wa kumpata mgombea urais ndani ya chama hicho.
 Walisema hivyo, baada ya kubaini kuwa kukatwa kwa jina la kada huyo ilikuwa ni mipango iliyopangwa kwa lengo la kuwanufaisha watu wengine.
Wakati wakipokea kadi za Chadema, vijana hao walisikika wakiimba wimbo unaosema ‘Bado wa wanamuamini Lowassa’ huku wakimtaka aungane nao katika chama hicho walichoingia ili wakakamilishe sfari yao ya matumaini.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Jimbo Kinondoni, Waziri Muhuzi, anawakaribisha vijana hao ili waweze kuungana na wezao kwa lengo la kukiondoa CCM madarakani na kuwaletea maendeleo wananchi.
Alisema licha ya vijana hao kutoridhishwa na mchakato huo, naye kada wa chama hicho, Kingunge Ngombale Mwiru alikaririwa navyombo vya habari kwamba alisekiktishwa na mnamna Kati ya Maadili ilivyoongozwa na viongozi wasiofuata maadilikatika kufanya uteuzi na kusababisha kuvuruga mchakato mazima wa uteuzi nadani ya chama hicho.
Alisema kutona kubaini ubabaishaji huo alimshauri Ngombale Mwiru kujiunga kujiunga na Chadema ili waweze kusimamia maadili nchini.
“Aige mfano wa mkongwe mwenzake wa siasa za Zanzibar, Hassan Moyo ambaye aliachana na CCM, hivi za sasa amekuwa akitoa ushauri kuhusu masuala ya Zanzibar,”alisema Muhuzi.
Awali, kiongozi wa kikundi cha Wanavyo hao, Michael Litanda, alisema kuwa wameamua kujiunga na Chadema kwa vile chama hicho ni basi la kuwapeleka sehemu fulani, wakati kwa upande wa CCM safari yake imefika kikomo.
“Tumezunguuka Tanzania nzima katika kuwashawishi wananchi wakubali kumdhamini kada wetu kwa hiyo, sisi baada ya kuvurugika mchakato ule tumehamia Chadema, kwa hiyo tunaomba aungane nasi,”alisema Litanda.

No comments:

Post a Comment