KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Wednesday, 20 January 2016

ASKARI ALIYEBAKA APANDISHWA KIZIMBANI



ASKARI wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), jijini Arusha, PC Raphael Paul (25), amepandishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Arusha kwa kosa la kumbaka mwanafunzi wa kidato cha sita Shule ya Sekondari ya Wasichana Korogwe.
Alisomewa mashtaka hayo jana mbele ya Hakimu Jasmine Abdul na Wakili wa Serikali, Sabina Silayo aliyedai mahakamani hapo kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa Januari 16 mwaka huu eneo la FFU kwa Morombo, jijini hapa na kumsababishia maumivu ya mwili.
Mwanasheria wa serikali alidai mahakamani hapo kwamba upelelezi wa shauri hilo umekamilika, Hakimu Abdul aliahirisha kesi hadi Januari 25 mshtakiwa huyo atakaposomewa maelezo ya awali.
Hata hivyo, Paul alikana shtaka hilo na kupelekwa mahabusu kwa kuwa kosa linalomkabili halina dhamana.

No comments:

Post a Comment