WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto, imesema Kanda ya Ziwa inaongoza kwa maambukizo ya
magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele (NTDs).
Miongoni mwa magonjwa hayo ni Usubi,
Trakoma, Kichocho, Minyoo, Mabusha na Matende.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es
Salaam jana, Mratibu wa magonjwa hayo kutoka wizara hiyo, Dk. Upendo Mwingira,
alisema kuwa serikali inaanza kampeni leo ya kutoa dawa ya kujikinga na ugonjwa wa kichocho kwa watoto wenye umri chini
ya miaka mitano kwa Mkoa wa Dar es Salaam.
Alisema kila baada ya mwaka mmoja wanatoa dawa
kwa watoto ya kujikinga na ugonjwa huo
inayoitwa Prazi Quantel.
Mwingira alisema kabla ya kupewa dawa hizo
watoto lazima wapewe chakula na wakae
muda wa saa mbili kisha wapatiwe dawa hizo.
“Ugonjwa wa kichocho huenezwa kupitia konokono na unasababishwa na minyoo ambayo
inaishi katika maji yaliyotuama na binadamu hupata maambukizo ya ugonjwa huo
mara baada ya kuogelea katika maji yaliyotuama,” alisema.
Alisema Tanzania iliridhia kudhibiti ugonjwa
huo kufikia mwaka 2020 na kazi hiyo inajikita zaidi kwenye umri hatarishi ambao
ni watoto wenye umri wa kwenda shule.
No comments:
Post a Comment