KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Saturday, 27 February 2016

UCHAGUZI WA MEYA WA JIJI WAAHIRISHWA KWA AMRI YA MAHAKA, POLISI WAPAMBANA NA MADIWANI WA UKAWA

sam1Polisi wakipambana na Madiwani wa UKAWA mara baada ya Uchaguzi huo kuairishwa tena leo kutoka na kesi iliyoko mahakamani iliyofunguliwa(Picha kwa hisani ya Fullhabariblog)
sam2
Mbunge wa Kibamba John Mnyika akiongea na Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema Freeman Mbowe kupata ufumbuzi baada ya uchaguzi kuahirishwa kwa amri ya mahakama.
sam3 Polisi wakiwa wamekaa kwenye jukwaa la juu wakifuatilia matukio katika uchaguzi huo ambao umeahirishwa kwa amri ya mahakama.
……………………………………………………………………………………………………………
VURUGU kubwa zimetokea wakati wa Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, mara baada ya uchaguzi huo kuairishwa  tena mwa mara ya tatu leo.
Baada ya kutokea vurugu hizo, Jeshi la Polisi lilivamia ukumbi wa Karimjee na kwa ajili ya kutuliza ghasia zilizotokea baada ya kuahirishwa kwa uchaguzi.
Uchaguzi  huo umeahirishwa baada ya kufunguliwa kesi Mahakamani hata hivyo,  Madiwani na wabunge waUmoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kupinga kuahirishwa kwa uchaguzi huo.
Tukio hilo la aina yake limetokea muda huu Jijini mara baada ya Mkurugenzi wa Jiji kutangaza kuahirishwa kwa uchaguzi huo kwa madai ya kusimamishwa na mahakamani, huku jambo hilo lilowachukiza madiwani wa Ukawa wakidai kuwa hawajapata barua hiyo ya kesi hiyo. 
Mara baada ya Ukawa kugomea hoja hiyo ndipo wakafikia hatua ya kutaka kufanya uchaguzi wenyewe, wakidai kuwa akidi ilikuwa  imetimia kwa ajili uchaguzi huo.
Kutokana na madai yao hayo,  wakaomba waendelee kufanya uchaguzi huo, jambo lililochukuliwa kuwa wanakaidi amri halali ya mahakama ya kusimamisha uchaguzi huo kutokana na kesi ya msingi iliyoko mahakamani.
Wakati wakijiiandaa kufanya uchaguzi huo Ukawa wenyewe, ndipo Polisi zaidi ya 15 wakaingia  ukumbini humo na kuwataka  madiwani   hao waachane na zoezi hilo na kuondoka ukumbini.
Kitendo hicho kiliwachukiza madiwani hao na kuanza vurugu  hali iliyowafanya Polisi kuanza kupambana na madiwani hao wa Ukawa  ili kuwatoa nje.

No comments:

Post a Comment