TAASISI ya Dream Success Interprises inatarajia kuzindua
shindano linalojulikana kwa jina la 'The African Master Mind Award',
ambapo mshindi wa jumla atajinyakulia tuzo yenye thamani ya sh. milioni 5, Octoba mwaka huu, uzinduzi huo utakaofanyika kesho mkoani Mbeya.
Hilo ni
Shindano la tatu tangu taasisi hiyo ilipoanzisha shindano hilo mwaka 2014 ambako washiriki walipatiwa
tuzo miongoni mwao alikuwemo aliyewahi kuwa CAG,
Ludovick Utouh, Vick Mtetema na Saed Kubenea.
Akizungumza na mwandishi, Ofisa Mtendaji
wa Tasisi hiyo, Charles Makoba, alisema shindano hilo linalengo la kuibua na kuwatunuku wale
wote waliyoonesha uadilifu katika kulitumikia Taifa.
Alisema lengo la Shindano hilo, ni kuibua fikra mbadala
zitakazochangia kumaliza tatizo la ajira nchini na barani Afrika kwa ujumla na
kuunganisha vijana wa bara hilo ili waweze kuwa na sauti moja katika kupigania
masilahi katika bara hilo.
Aidha, Makoma, alisema washiriki wote watakaoshiriki
shindano hilo
wtatoa hotuba fupi ya muda wa dakika kumi kwa kila mmoja.
Akizungumzia uzinduzi huo, Mkurugezi wa Mipango wa
taasisi hiyo, Joshua Laurence, alisema maandalizi yamekamilika na washiriki
wote wako tayari kwaajili kesho.
"Tukimaliza hapa Mbeya uzinduzi utaendelea katika
mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma,
Mwanza na Arusha, "alisema Laurence ambaye yuko mkoani Mbeya.
Alisema uzinduzi katika mikoa hiyo unalenga kupata
washiriki 10 ambao wataingia katika hatua za mwisho za kumpata mshindi wa Taifa
kwa ujumla ifikapo Okotoba mwaka ambapo siku hiyo itakuwa Ile ya Kumbukumbu ya
kifo cha Baba wa Taifa hayati Julius Nyerere.
"Shindano hili pia litaboresha uchumi wa Watanzania
kwa kuwaanzisha kampuni za fani mbalimbali walizosomea ikiwemo ujuzi unaotokana
na vipaji na hiyo itakuwa ni moja ya msaada wa utekelezaji wa hotuba ya Rais
John Magufuli, "alisema Laurence.
Lawrence, aliwataja waandaji wazalishaji wa virutubisho lishe
vya Tangreen Juice na Blue Juice.
No comments:
Post a Comment