KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Monday, 29 February 2016

WAFANYABIASHARA WA NYAMA KATIKA SOKO LA VINGUNGUTI WAMUOMBA WAZIRI MWIGULU KUINGILIA KATI MGOGORO WAO



Umoja wa Wafanyabiashara wa Mifugo na Mazao yake Vingunguti (Uwamivi Society),katika machinjio ya Vingunguti, wilayani Ilala, wamemtaka Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba kuingilia kati mgogoro wa ndani ya umoja huo, ambao unaikosesha serikali mapato.
Baadhi ya wanachama wamefichua siri ya machinjio hiyo ya ukusanyaji wa mapato kidogo ukilinganisha na mifugo inayoingizwa manjioni hapo kuwa kumechangiwa na mfumo mbovu unaolelewa na Mkurugenzi, wa wilaya hiyo, Isaya Mngurumi.

Hayo yalifichuliwa jijini Dar es Salaam juzi, wakati wafanyabiashara wa machinjio hiyo walipozungumza na wandishi wa habari kuhusu    matumizi mabaya ya fedha za miradi huo, yanayofanywa na uongozi wa Uwamivi.
Akielezea sakata hilo, Prasidus Mbita alisema viongozi wa umojaa huo wametungwa sheria za kuhakikisha kila mfanyabiashara anaingiza ng'ombe wawili hata kama ana uwezo wa kuingiza zaidi ya hao.

"Pindi wafanyabiashara wanapozidisha mifugo zaidi ya hiyo vingozi wa umoja huo unakusanya sh. 10,000 kwa kila ng’ombe mmoja aliyezidi huku fedha hizo zikiingia mifukoni mwao hali inayoikosesha serikali mapato.
 "Utaratibu huo wa kulazimisha wafabiashara kuchinja ng'ombe wawili wakati mwingine pia kunasababisha upungufu wa nyama sokoni hivyo kufanya bei ya nyama kupanda," alisema Mbita.
Mbita, alisema kutokana ubadhirifu huo ulisababisha baadhi ya waliokuwa wanachama wa umoja huo wanaofikia 55 kujitoa na kumuandikia malalamiko kwa Mkurugenzi ili kumfahamisha namna mapato ya serikali yanavyohujumiwa na majipu.
"Lakini cha kusikitisha baada ya kutuma barua hiyo Mkurugenzi alitoa jibu la kutukatisha tamaa kwa kututaka wafanyabiashara wote kukubali kuchangia umoja huo," alisema Mbita.
Akizungumza sababu za wao kujitoa kwenye umoja huo, Mailo Machage alisema pamoja na kuwa ndani ya umoja huo kwa miaka mitano wakichangishwa fedha za mauzo ya damu ya wanyama hata hivyo, hawaoni kwa namna gani watanufaika na umoja huo.
"Kwa siku tunachangia pipa 20 zenye thamani ya sh. 600,000 lakini tunapohoji mapato na matumizi eti tunaambiwa fedha zitakazopatikana

zitapelekwa kwa watoto yatima," alisema Machage.

Naye Othman Kailo aliongeza kuwa hata baada ya kujitoa umoja huo umeendelea kuwatoza michango na hata walipotaka kurudishiwa michango waliyochangia walikataliwa.

Alipotafutwa Mwenyekiti wa umoja huo Anatolio Lubeleje alikana kuwepo kwa madai hayo na kusema kwamba kila mwaka wamekuwa wakifanya mikutano na kusoma mapato na matumizi.

Akijibu  malalamiko hayo Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Isaya Mngurumi, aliwashauri wanachama hao kuwa kama wanahisi wanafanyiwa mambo kinyume na katiba wajitoe katika chama hicho na kuunda umoja wao ambapo manispaa itashirikiana nao kwa kuwapa viongozi wa kuwasimamia.
Alisema wakati mgogoro huo unachipua alikutana na uongozi na wadau hao kwa pamoja wakakubaliana kila mfanyabaishara atachinja ng’ombe kulingana na orodha ya wateja wake na sio vinginevyo.

“Kama leo wanalazimishwa kuchinja ng’ombe wawili hilo ni kosa na haliko katika katiba yao, kwa sababu kama mahitaji ya nyama ni makubwa kwa nini wapangiwe kiasi cha kuzalisha bidhaa? Nawashauri watafute katiba ya chama chao waisome kwa makini watafute ufumbuzi haraka bila hivyo watakatana mapanga,” alisema Mngurumi.

Alifafanua kwamba chama hicho kimesajiliwa na serikali Septemba 2012, kwa nembo ya picha ya Ng’ombe, Mbuzi , Kondoo na Ngozi.


No comments:

Post a Comment