UMOJA wa Mafundi Magari wilayani Kinondoni jijini Dar es
Salaam wameapa kutoondoka katika eneo wanalofanyia kazi kwa madai ya kumpisha
mtu aliyetajwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kuwa ni
muwekezaji wa eneo hilo.
Kauli hiyo inakuja siku chache baada ya Kaimu Kamishna wa
Ardhi, Makondo kuwataka kuondoka katika eneo hilo kwa masharti ya kugawana eneo
hilo la hekar 32 nusu kwa nusu.
Akizungumza kwenye
mkutano ambao walitarajia kukutana na Meya wa Manispaa ya Kinondoni Boniface
Jacob, ambaye hata hivyo hakutokea kutokana na kutingwa na majumu mengine,
Naibu Katibu wa Umoja huo, Gratia Mbelwa, ambaye ni Mwenyekiti wa Serikali ya
Mtaa Madale kupitia (CCM), alisema kinachofanywa na wizara hiyo ni kiini macho
ambacho hawako tayari kukikubali.
Alisema agizo la wizara wizara hakitekelezeki kwa vile
utaratibu wa kufikia maamuzi hayo ulikuwa wakibabe ambao umetolewa zaidi kwa
kujali masilahi ya mtu huyo ambaye hawamfamu tangu kuanza kwa mgogoro huo kwa
zaidi ya miaka 10 sasa.
Mbelwa, alisema wameshangazwa na barua ya Kamishna huyo wa
Ardhi kwa kudai kuwa ili kumaliza mgogoro huo ni lazima pande mbili
zinazovutana kubaliana na uamuzi uliyofikiwa katika mazungumzo kati yao kwa
pamoja.
Aliyataja mapendekezo hayo kuwa ni muwekezaji aliyetajwa kwa
jina la Nyanza Roads Works aachie ekari 16 kutoka kwenye eneo hilo lao
wanalomiliki kisheria.
Vilevile umoja wa Mafundi hao waondoe miundombinu yao
iliyoko katika eneo hilo na kuipeleka kwenye eneo la ekeri 16 watakaotengewa.
Kingine kilichoanishwa kwenye barua hiyo, ni Wizara ya Ardhi
kwa kushirikiana na Manispaa ya
Kinondoni wamege ekari hizo 16 kisha kuzipima, kuonesha na kuwamilikisha umoja
huo wa mafundi magari (Tegeta Magereji).
Pia Kamishna huyo katika barua hiyo amemtaka Nyanza Roads
Works kurejesha Hata halisi (CT.NO.29971) kwa Kamishna wa Ardhi ili zoezi tajwa
hapo juu liweze kukamilika.
“Tunataka kuifahamisha Wizara ya Ardhi, kuwa hawako tayari
kuondoka kwa masharti hayo kwani wakati uwamuzi huo baadala yake tunamtaka
waziri wa wizara hiyo Wiliam Lukuvi kutembelea eneo hilo na kujionea hali
halisi kama kweli hicho kinachodaiwa kinawezekana,”alisema Mbelwa.
Alisema, kuwa Wizara inapaswa kuheshimu uwamuzi wa Manispaa
ya Kinondoni ambayo inaamini kuwa eneo hilo ni la mafundi kutokana na
makubaliano ya awali wakati wanakabidhiwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Yusuf
Makamba.
Awali, Mwenyekiti wa Umoja huo, Alawi Kassimu, alipokuwa
akiwasome maagizo hayo ambayo alidai kuwa wakati walipokutna na Kamishna huyo
walitakiwa kubali mapendekezo hayo bila ya kutoa hoja.
Hata hivyo baada ya kuisoma barua hiyo mafundi walichangia
mapendekezo hayo kwa muunkari ya juu wakipinga agizo hilo.
Kitendo hicho kilimfanya mwenyekiti huyo kuwataka mafundi wenzake
kupunguza jazba wakati wanapojadili suala hilo kwani kunaweza kuwafanya
waonekane wakorifi na kukosa haki yao.
No comments:
Post a Comment