KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Thursday, 3 March 2016

BODI YA BARABARA YAKUTANA JIJINI DAR ES SALAAM

KIKAO cha Bodi ya Barabara  zilizo chini ya Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), kimeingia dosari baada ya wabunge sita wanaotoka vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kususuia kuhu ,mbunge wa Kinondoni Maulid Mtulia, akihudhuria.
Wabunge waliosusia kikao hicho ni Abdallah Mtolea, Said Kubenea, John Mnyika, Anatropia Theopist na Halima Mdee, Mwita Waitara ambao walipandishwa kizimbani.
Alipotawa Mtulia kufahamu mbona amehudhuria kikao hicho huku msimamo wa Umoja wao ukiwa ni kususia ambapo alisema, ushiriki wake katika kikao hicho haikuwa makusudio yake bali kulichangiwa na mawasiliano dhaifu baina yake na wenzake.
“Unajua suala hili linagusa sehemu tatu kwanza kuna upande wa wananchi waliyonichagua, kuna masilahi ya chama na huu umoja wetu, sasa ningeapewa taarifa hata hivyo ingebidi tujadiliane kabla ya kuchukua uamuzi,”alisema Mtulia.
Alisema hata juzi wakati wenzake wanasusia ziara ya kutembelea miradi yeye hakwenda lakini siyo kwasababu ya ya msimamo wa Ukawa bali kwakuwa hakuwepo na hakuwa na taarifa hiyo.
Hata hivyo, Mtulia alisema kama angepata taarifa mapema asingeshiriki na kwamba kilichotokea ni bahati mbaya, baada ya kumaliza kuzungumza na wandishi wa habari alitoweka katika Kikao hicho.
Hata hivyo, kuhudhuria kwa Mtulia kulisababisha akidi ya wajumbe kutimia kwani walifika saba kati ya 12 hivyo kumchangua Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo.
Aliyeshinda nafasi hiyo ni mbunge wa Ilala, Mussa Zungu, baada ya jina lake kupendekezwa na Mbunge wa Kigamboni Faustin Ndugulile, kisha kupitishwa na Wabunge hao wachache wa mkoa wa Dar es Salaam wa CCM.
Ukawa juzi wakati wakisusia ziara ya kutembelea miradi ya barabara jijini walisema hakuna haja ya kushirikiana na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutokana na uhasama uliyojitokeza hususani baada ya tukio la kuahirishwa uchaguzi wa Meya Februari 27, mwaka huu.
Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadik, amesema Mkoa huo umetengewa zaidi ya sh. bilioni 343 kwa ajili ya ya mipango ya matengenezo ya barabara katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2016/2017.
Akizungumza kwenye Kikao hicho, Sadiki, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo, alisema lengo kuu la bodi ya barabara ya mkoa ni kuratibu, kushauri na kufuatilia maendeleo ya miundombinu ya barabara katika mkoa huo.
Alisema kuwa kuna haja ya watendaji wote kujiepusha na matumizi ya fedha hizo na kwamba kila takayekwenda kinyume na matumizi ya fedha hizo hatavumiliwa na hatua kali dhidi yake zitachukuliwa.
“Ni matumaini yangu kuwa kiasi hiki cha fedha kitatumika kama ilivyokusudiwa ili kupata thamani halisi ya fedha hizo, matumizi thabiti ya fedha hizo zitasaidia kwa kiasi kikubwa kukabiliana na baadhi ya matatizo yaliyopo ya miundombinu ya barabara za mkoa wetu,”alisema Sadik.
Sadik, alisema anatahadharisha hivyo, kwa vile kumekuwepo na baadhi ya mamlaka ambazo hazipendi kuzingatia taratibu na miongozo ya matumizi ya fedha zinazotolewa kwa ajili ya miradi hiyo, huku akibainisha kuwa  haikubaliki.
Aliwaagiza na kuwataka wasimamizi wa miradi ya matengenezo ya barabara kuzingatia taaluma na weledi husika ili kupata thamani ya fedha kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu husika bila kukiuka sheria ya manunuzi.
Temeke
Aidha, wakati wakijadili nafaniki na mipango ya maendeleo kwa upande wa Temeke, Sadiki alimuagiza Mkurugenzi wa manispaa hiyo hadi ifikapo Jumatatu ijayo ahikikishe anamfikishia taarifa kuhusu maeneo yote ya wazi ambao umiliki wake hauweleki.
Alisema maeneo hayo yanadaiwa kuwa yana wamiliki wake lakini cha kushangaza kwa muda mrefu hayajaendelezwa huku serikali Manispaa ikikosa maeneo kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya wananchi.
“Niwapongeze Temeke kwa hatua yenu ya kununua mashine kubwa kwa ajili ya kufanyia usafi hata hivyo jaribuni kusimamia miradi mingine ili iweze kukamilika,”alisema Sadik.
Mkuu wa wilaya hiyo Sofia Mjema, aliiomba Wakala wa Barabara Tanzania (Tanrods) kukamilisha barabara zote ambazo wamezianza kwani iko baadhi ya miradi imechukua muda mrefu bila ya kukamilika kwa wakati.
 Kinondoni
 Kwa upande wa wilaya hiyo, Sadiki alimuagiza Mkurugenzi kuwa anahakikisha kuwa anasimamia shuguli ya kuwadhibiti watu wote wanaotaka kurejea katika maeneo ya mabondeni baada ya kuondolewa hivi karibuni.
“Maeneo haya ni hatarishi hivyo ni lazima mhakikishe kuwa kila aliyeondolewa katika maeneo hayo harejei tena, na ieleweke serikali haina uwezo wa kuwapatia viwanja wananchi hao kwani ni gharama kubwa,”alisema Sadiki.
Sadik, alitoa msimamo huo baada ya Wabunge Bonah Kalua na Maulid Mtulia kuitaka serikali kuwasaidia viwanja wakazi hao kwa vile ni masikini na wanahitaji msaada.
Pia, aliagiza uongozi wa Halimashauri hiyo kuwa inawaondoa wafanyabiashara ndogondogo katika eneo la ubungo na kuwapeleka katika Kituo cha Mabasi Simu 2000.
“Nashangaa kituo kile kimetumia mamilioni ya shilingi lakini nashangaa mnakataa kukitumia, hakikisheni mnawaondoa kwani ni hatari kwa wafanyabiashara hao wanaoning’iniza biashara zao kweye mashine ya kupoozea umeme (transphomer),”alisema Sadiki.
Ilala
 Mkuu huyo wa Mkoa, baada kusikiliza matatizo ya uharibifu wa barabara za Halmashauri, unaofanywa na baadhi ya magari yenye uzito mkubwa wa ukilinganisha uwezo wa barabara hizo zenye uwezo wa kuhimili uzito wa tani saba, kwanza aliomba alezwe ni nani anahusika katika utoaji wa vibali kwa gari hizo kuungia katikati ya jiji.
Hata hivyo, Wakurugenzi pamoja na watendaji wao wote walishindwa kumtaja mhusika, hali iliyomfanya atowe uamuzi mgumu ambao ulikuwa ni kufuta vibali vyote vyote vinavyoruhusu gari zenye uzito wa zaidi ya tani kumi.
Alisema kuanzia jana mtu yeyote, atakayekaidi agizo hilo atakuwa amevunja sheria hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Aliwataka wakurugenzi na watendaji wake wote kuwa wakali katika kusimamia hilo kwani bila ya kufanya hivyo barabara za halimashauri zitaendelea kuharibika hukku wakiendelea kuiomba serikali msaada.
“Halmashauri zote hakikisheni magazri hayo yenye uzito zaidi ya tani kumi hayapiti kwenye barabara zetu za halmashauri hii itatusaidia kuzuia uharibifu,”alisema Sadiki.
Awali Mbunge wa Ilala, Mussa Azan Zungu, alisema uharibifu huo ulikuwa ukichangiwa na utolewaji vibali vya magari yenye uzito mkubwa kuingia katika barabara uwezo wa kuhimili uzito wa kuanzia tani tano hadi kumi.

Alisema, kama hakutakuwa na ushirikiano wa kusimamia miundombinu hiyo ya halmashauri za wilaya basi zitaendelea kulalamika huku barabara hizo zikiendelea kuharibiwa.

No comments:

Post a Comment