OFISA Usafirishaji wa Manispaa ya Halmashauri ya Muheza,
George Masatu, ameingia matatani baada ya kudaiwa kutumia magari mawili ya
ofisi kwa ajili shughuli zake binafsi jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya halmashauri hiyo
kilidai kuwa serikali inapaswa kudhibiti matumizi ya magari hayo kwa kuwa
kimekuwa chanzo cha kuongezeka kwa matumizi ya serikali.
Kilidai kuwa matumizi ya ofisa huyo yamechangia gharama
za uendeshaji wa magari hayo hususani matumizi ya mafuta.
Chanzo hicho kilitaja magari yanayotumiwa katika
shughuli za ujenzi wa nyumba ya ofisa huyo ni SM 5581 na SM 3924 Toyota pickup.
“Kama serikali inapambana ili kudhibiti mishahara hewa
katika halmashauri zetu basi pia itambue kuna jipu jingine linaloongeza
matumizi ni shughuli binafsi za baadhi ya maofisa kama Masatu,” kilidai.
Akizungumzia tuhuma hizo Masatu alisema ndiyo kwanza
anazisikia taarifa hizo hivyo hawezi kuzungumzia chochote huku akidai kuwa
taarifa hizo zinatokana na chuki binafsi.
“Wakati mwingine hebu tujiongeze, hivi kweli gari hizo
zinaweza kubeba mzigo mzito, acha nikwambie kuwa sijawahi na sitajafanya
kitendo hicho,” alisema Masatu.
Masatu aliwashangaa waliotoa taarifa hizo na kuwaita
kuwa ni watu wenye chuki binafsi kwani uhusiano wake wa kikazi na wafanyakazi
wenzake ni mzuri.
No comments:
Post a Comment