MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),
imesema ununuzi wa wa matishari tatu kwa ajili ya upakiaji na upakuaji mizigo
katika Bandari ya mkoani Tanga, ulipata baraka zote za Bodi ya Wakurugenzi.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jijini
Dar es Salaam jana, na kusainiwa na Menejmenti ya TPA, ilieleza kuwa mchakato
wa kununua matishari hizo ulianza mwaka 2010/11 baada ya aliyekuwa Mkuu wa
Bandari kwa wakati huo, kuandika barua kwa Mkurugenzi Mkuu kukunuliwa matishari
hayo matatu ya tani 300.
Kwa mujibu wa Menejimenti matishari hayo,
yalinunuliwa baada ya shehena ya mizigo kuongezeka katika bandari hiyo ya
Tanga.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa matishari hayo
yalinunuliwa baada ya maombi ya kuzinunua kupitishwa na Bodi ya Wakurugenzi, wa
viwango vya ubora (Technical Specification).
“Uamuzi ulipitishwa kwa ajili ya ununuzi wa
tishari (barges) mbili, viwango viliandaliwa na Kurugenzi ya Uhandisi na
kuwasilishwa katika Kitengo cha Ununuzi kwa ajili ya kuanza mchakato wa zabuni
Februari 2011,”ilieleza taarifa hiyo.
Aidha, tangazo la zabuni ya ununuzi wa matishari
lilitoka Februari 28, 2011 na Machi Mosi kupitia magazeti ya the Guardian na
Machi Mosi, 2011, likatoka kwenye gazeti la serikali Daily News, Machi Mosi na
Mbili mwaka huo huo wa 2011.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa ilipofika Aprili 28,
2011 zabuni zilifunguliwa na jumla ya wazabuni nane walijitokeza kwa kupeleka
maombi yao.
Baada ya ufunguzi wa zabuni Kamati ya
Uchunguzi wa Zabuni iliundwa na
Mkurugenzai Mkuu na ilijumuisha ‘Marine Engineer’ kutoka Bandari ya Tanga
ambaye kwa kipindi hicho alikuwa amehamishiwa Bandari ya Dar es Salaam.
Ilifafanua kuwa baada ya uchambuzi wa zabuni
kukamilika Bidi ya Zabuni, iliamriwa kwamba Kamati ya uchunguzi iundwe ili
kwenda kufanya ‘due diligence’ kwenye kiwanda cha mzabuni aliyependekezwa
kufanya kazi hiyo kabla ya kupewa zabuni hiyo.
Baada ya uchunguzi Kamati hiyo ya uchunguzi
ilifanyakazi yake na kupeleka taarifa kwamba walijiridhisha kuwa kampuni hiyo
ilikuwa na uwezo wa kufanya kazi hiyo.
Menejimenti hiyo, ilifafanua kuwa baada ya
uchambuzi huo wa kina pamoja na kupitia taarifa ya uchunguzi, Bodi hiyo ya
Mamlaka ya Bandari iliidhinisha zabuni kutolewa kwa kampuni itwayo John Achelis
anda Sohne Gmbh ya Ujerumani katika kikao chake maalum Na. 135 kilichafanyika
Desemba Mosi na Mbili mwaka 2011.
Ilieleza kuwa Januari 10 mwaka 2012 Mkurugenzi
Mkuu alitoa barua ya kupewa John Achelis anda Sohne Gmbh, kwa ajili ya
kutengeneza matishari matatu ya ukubwa wa tani 3500 kila moja kwa gharama ya
dola za Kimarekani 10,113,00.
Makubaliano hayo yalikuwa matishari hayo
yatengenezwe kwa na hatimaye mkataba wa manunuzi wa matishari hayo ukasainiwa
ukasainiwa mnamo Machi 2, 2012.
Baada kikao hicho mkataba ulisainiwa, Mshitiri
(Supplier), alipeleka michoro kwa ajili ya kutumika katika ujenzi wa matishari
hizo huku akiomba uidhinishwe na mamlaka ya bandari kabla ya kuanza
utengenezaji.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa michoro hiyo
iliidhinishwa na Mkurugenzi wa Uhandisi.
Kulingana na mkataba matishari hayo yalitakiwa
yajengwe kwa kuzingatia ubora wa kimataifa chini ya usimamizi wa Bureau
‘Veritas’ (B/V) na yalijengwa kwa ubora huo na kuidhinishwa na B/V.
Aidha, Mshitiri alitakiwa kusafirisha matishari
hayo kwa kupakiwa katika meli, hata hivyo matishari hayo hayakupakiwa kwenye
meli na baadala yakeyalivutwa kwa kutumia boti kwani John Achelis and Sohne
Gmbh.
Mshitiri aliomba kubadili kubadilisha njia ya
usafirishaji kuwa wa kuvutwa kwa boti baadala ya kupakiwa kwenye meli na TPA
iliridhia matishari hayo yavutwe baadala ya kupakiwa melini na yalikatiwa bima
ya kusafirisha kwa njia hiyo.
Wakati wa usafirishaji njiani yalikumbana na
dhoruba ya kimbunga kikali baharini na kusababisha boti iliyokuwa ikiyavuta
matishari hayo kuzama na kufanya matishari hayo kugongana kwa kupigwa na
mawimbi na kusukumwa hadi nchini Malaysia yalipokwama kwenye tope na mikoko.
Ilieleza kuwa ajali hiyo ilisababisha matishari
hayo kupata uharibifu.
Kwa kuwa maishari hayo yalikatiwa bima, ya
kusafirisha kwa njia ya kuvuta na yakapata ajali iliyosabaisha uharibifu huo,
gharama za matengenezo ya matishari hayo zikabebwa na bima iliyokatwa.
Kabla ya matengenezo hayo kufanyika Surveyor wa
B/V, alifanya ukaguzi wa uharibifu na kuruhusu matengenezo yafanyike kwa kila
tishari kulingana na uharibifu wake.
Taarifa hiyo inaonesha wakati wa matengenezo
wataalamu wa TPA walifanya ukaguzi mara mbili wakati matengenezo hayo
yakiendelea na pia baada ya utengenezaji kukamilika na kuridhiwa na Mkaguzi
B/V.
Baada ya matengenezo hayo, matishari hayo
yalivutwa na kuletwa bandari ya Tanga Agost mwaka 2014 na baada ya kufanyiwa
ukaguzi yalionekana kuwa na kasoro chache kama vile kutokuwepo na fenders zenye
uwezo wa kuzikinga wakati wa maegesho melini ama gati.
Pia yalikuwa hayana mifuniko ya Falk ‘Hatch’
kuwa si rafiki katika shughuli za kupakia na kupakuwa, na Mshitiri alitakiwa
kufanya marekebisho kwa gharama zake kwa kuwa tishari hizi zilikuwa bado
hazijajaribiwa na kupokelewa na TPA.
Taarifa hiyo ilifafanua kuwa baada ya kufanyiwa
majaribio yalfanywa, Agosti 3, 2015 kwa kupakia shehena ya coal toka kwenye
meli ya African Griffon.
Katika mkataba ilielewekwa wazi kuwa matishari
hayo yakifika Tanga yafanyiwe majaribio ili kuangalia uwezo na tabia ya
matishari hayo yakiwa ya yamejazwa shehena.
Majaribio hayo yalionesha kuwa matishari hayo
yalikuwa imara wakati yalipopakiwa mizigo na kuweza kuvutwa hadi kwenye gati na
kupakuliwa mzigo huo.
Taarifa hiyo, ilieleza kuwa matishari hayo
yaliendelea kufanyiwa majaribio kwa kuhudumia meli tatu ambazo ni African
Griffon iliyofika bandarini Tanga Agosti 31, 2015, Diamomond Sky Desemba 04, 2015 na Thor Breeze iliyofika
Januari 12, 2016.
“Wakati matishari hizo yakifanya majaribio
matatizo yafuatayo yalijitokeza wakati wa upakuaji wa shehena, ambazyo ni
ukubwa wa matishari umesababisha krini za meli kushindwa kupanga mizigo vizuri
hivyo kulazimu kuhitajika kwa ‘wheel loaders’ ambazo tayarimchakato wa ununuzi
wake umeanza.
Tatizo jingine ni Tug Boat’ kubwa inahitajika
kwa ajili ya kukokota matishari hayo na tayari mamlaka imeagiza na inatarajiwa
kuwasili Tanga Juni mwaka huu.
Kutokana na matatizo yaliyojitokeza Mshitiri
alitakiwa kurekebisha ‘hatch cover’ kama ilivyokubalika wakati wa majaribio na
ndiyo maana hadi sasa hajalipwa kiasi chake cha fedha ambacho ni dola za
Marekani 1,348,400.
Kwa mujibu wa mkataba kiasi kilichobaki
kinapaswa kulipwa baada ya majaribio kufanyika kwa mafanikio na kupewa
‘Certificate Acceptance’ ambayo hadi sasa hajapatiwa.
Taarifa hiyo inaonesha kuwa TPA inapenda
kuwahakikishia watumiaji wa Bandari kwamba inaendelea kuboresha miundombinu na
vifaa ili kutoa huduma zilizo bora na za viwango.
No comments:
Post a Comment