KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Saturday, 12 March 2016

WAZAZI KUHAMISHA WATOTO KATIKA SHULE YA BINT MUSSA KWA MADAI YA KUTOFUNDISHWA



BAADHI ya wazazi wenye watoto wanaosoma kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari ya Binti Mussa, wilayani Ilala, wako mbioni kuwahamishia watoto wao katika shule nyingine, kwa madai ya wanafunzi hao kutofundishwa masomo ya Siyansi tangu walipojiunga na muhula wa masomo mwaka huu.
Halikadhalika wazazi hao wameushutumu uongozi wa shule hiyo kwa kushindwa kusimamia vizuri michango  ya wazazi kwa ajili ya kununua madawati hadi kusababisha wanafunzi kukali visafleti vilivyojazwa mchanga  kama madawati.
Naye Mkuu wa Shule hiyo Fadhil Mbata amesema wazazi wanaodai hivyo ni wale wasiyopenda kuhudhuria vikao vya wazazi vyenye lengo la kujadili maendeleo ya shule hiyo.
Hayo yalisemwa na wazazi jijini Dar es Salaam leo, wakati walipokuwa akizungumza na  wandishi wa habari kuhusu malalamiko hayo ambayo hivi sasa yamefikia hatua mbaya ambayo inaweza kuangusha kiwango cha ufaulu wa watoto wao.
Mmoja wa zazi hao, Khamis Juma, alisema wamefikia hatua hiyo baada ya kubaini kuwa chanzo cha  matatizo hayo kinachangiwa na Mkuu wa Shule hiyo ambaye ameshindwa kuwalipa walimu wanaofundisha masomo hayo kwa mkataba.
Alisema, kutokana na mazingira hayo wameona ni vema wakawamisha watoto wao kwenda katika shule wanazoamini kuwa watoto hao watafundishwa na kujihakikishia ufalu wao katika mitihani yao.
Juma alisema hivi sasa watoto hao wanakabiliwa na mtihani kwa ajili ya mapuniziko mafupi ya mwezi watatu lakini cha kushangaza wanafunzi hao tangu walipojiunga na muhula wa masomo ya kidato cha kwanza mwaka watoto hao hawajafundishwa somo la bioloji kiasi hawajui siku ya mtihani watajibu nini.
Aidha, baada ya Mkuu huyo wa Shule hiyo kuona wimbi la wazazi kuhamisha watoto linaongezeka hivi sasa ameamua kuzuia utaratibu huo kwa kuwaeleza wazazi kuwa Ofisa Elimu wa Wilaya amepiga marufuku uhamishaji huo wawatoto katika shule hiyo.
“Kwa mfano kuna mwalimu aliyekuwa akifundisha somo la Bioloji na ambaye ameisaidia ufaulu wa somo hilo katika mtihani uliyopita lakini cha ajabu mwalimu huyo hajalipwa malipo yake kwa zaidi ya mwaka haliyomfanya ashindwe kuendelea na kufundisha somo hilo,”alisema Juma.
Alisema baada ya Mkuu huyo kuona deni la mwalimu huyo linazidi kukuwa ikabidi aachane na mwalimu aliyekuwa akifundisha somo hilo la bioloji huku akiamua kufundisha masomo yote ya sayansi huku akikabiliwa na majukumu ya uongozi kitendo kinachomfanya ashindwe kuingia darasani kwa wakati.
Hata hivyo, pamoja nakuogopa deni la mwalimu huyo kukuwa, sasa ameamua kufanya ujanja wakufundisha masomo hayo, huku akiandika madai ya kulipwa kama vile mwalimu wa mkataba jambolo linamfanya awakoseshe vipindi wanafunzi hao.
Madawati
Naye Fatuma Charles, alisema kuwa uongozi wa shule hiyo unaongoza kwa matumizi mabaya ya michango ya madawati kutoka kwa wazazi ambao walijitolea kuchangia katika kipindi cha mwaka 2013 hadi mwaka jana.
Alisema baada ya kushindwa kutumia michango hiyo vizu, kumefanya watoto kukalia viroba walivyovijaza mchanga kama vile ndiyo madawati.
“Kuna wenzetu wanahamisha watoto wao lakini mimi nasema sitamhamisha mwanangu bali nitapambana na uongozi wa shule kwa lengo la kuisaidia shule hii kwa sababu kumhamisha mtoto siyo ufumbuzi wa tatizo na vipi kwa wale wasiyokuwa na uwezo watafanyaje,”alisema Fatuma.
Akizungumzia malalamiko hayo, Mkuu wa Shule hiyo,  Mbata alisema kuwa kukosekana kwa walimu hao wa sayansi kumetokana na wazazi wenyewe kushindwa kulipa madeni ya walimu hao waliyokuwa wakifundisha masomo hayo ya zaiada (Parttime).
Alisema kuingia kwake kwenye vipindi siyo kama amejirundikia vipindi ama anajilipa bali anaingia kwa dharula na hiyo intokana yeye kupenda kuona watoto hao wanakaa darasani bila ya kufundishwa.
Mbata, alisema kutokana na mazingira hayo hata weza kuendelea na kuingia darasani ila alichofanya ni kupeleka taarifa  kwenye ngazi husika kwa ajili ya kuongezewa walimu ambapo hatua za utekelezaji zimekwishaanza.
“Suala la ngono kati ya wanafunzi na walimu kama mzazi ana taarifa za kutosha basi azifikishe kwenye kamati ya shule ili mhusika achukuliwe hatua hivi kama mwalimu anafanya hivyo basi huyo hana sifa tena ya kuitwa mwalimu ni wakufukuzwa tu,”alisema Mbata.
Akizungumzia madawati, Mbata, alisema michango ya wazazi imetumika kama ilivyokusudiwa na wala siyo kweli kama kuna wanafunzi wanakalia viroba vilivyojazwa mchanga ingawa kweli hapo awali yalikuwepo matatizo hayo.

No comments:

Post a Comment