RAIS John Magufuli amezua mjadala baada ya kuvamia Tawi la
CRDB (Holland Branch), akiwa kwenye gari namba T 182 DFQ huku likiwa halina
nembo ya adamu na hawa wala bendera.
Tukio hilo lililochukuwa dakika 25, limetokea majira ya
asubuhihi jijijni Dar es Salaam jana katika tawi hilo ambalo liko katika
makutano ya Barabara ya Ohio na Samora bila kutarajiwa.
Mara baada ya Rais
Magufuli kufika katika eneo liliko tawi hilo makutano ya barabara hizo yalifungwa
huku ndipo rais aliposhuka kwenye gari na kuingia ndani ya benki hiyo.
Wakati akikaribia kuingia ndani ilibidi baadhi ya wateja waliyokuwa
awakijiandaa kuingia ndani ya benki hiyo ilibidi wazuiwe kuingia huku huduma
ikiendelea tu kwa wale ambao waliyokwisha ingia.
Aidha, baada ya kuingia ndani baadhi ya wateja wa tawi hilo
na wananchi wengine walibaki wakishangaa huku wengine wakijiuliza imekuwaje
Rais kuingia benki kwa sitaili ile kwani baadhi ya wananchi kudai kuwa
hawajaona tukio kama lile kwa marais wote waliyopita.
James Charles, ambaye ni dereva wa Tex, alisema baadhi ya
wananchi waliyokuwa kwenye eneo hilo baada ya kuona ulinzi unaimalishwa
walishtuka lakini mara walimuona Rais Magufuli akishuka kwenye gari hali
iliyowafanya wafikirie anakwenda kutembelea ofisi yake ya zamani.
“Lakini kufumba na kufumbua tukamuona anaelekea kwenye
benki ya CRDB tukajiuliza vipi rais leo kaamua kuwa kama mteja hata hivyo hatujui
kama hiyo ilikuwa inawezekana.
Lazima kutakuwa na kitu haiwezekani aende akachukue fedha
kwa utaratibu ule ngoja tusubiri tutasikia amefuata nini,”alisema Charles.
Joyce Godwin ambaye ni mwanafunzi wa moja ya chuo kimoja
cha elimu ya juu, alisema kuja kwake kumewashtua wafanyakazi wa tawi la benki
hiyo kwani anadhani wanadhani rais alikwenda pale kwa ajili ya kutumbua majipu.
“Mimi nwakati Rais Magufuli anaingia nilikuwepo ndani kwenye
foleni nikisubiri huduma kwa ujumla kila mmoja wetu alishituka lakini hatukujua
kilichomleta,”alisema.
Wandishi,wali jaribu kutaka kujua kilichompeleka Rais
Magufuli pale kwa kuwauliza baadhi ya wafanyakazi wa tawi hulo hata hivyo
hakuna aliyekuwa tayari kuzungumzia ujio huo kwani nao hawakuwa wakijua
chochote.
Baada ya Rais Magufuli kumaliza kazi yake iliyompeleka
alitoka na kuingia kwenye gari lake kisha wakati akiondoka alishusha kioo huku
akichungulia nje na kuwapungia mkono wananchi.
No comments:
Post a Comment