KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Thursday, 26 February 2015

WAKAZI DAR WAILALAMIKIA SERIKALI

BAADHI ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wameomba serikali kutoa ufafanuzi kuhusu ubomoaji wa vipande vya Barabara ya Mradi wa Magari ya endayo Haraka (DART) vilivyokamilika, kitendo kinachosabaisha foleni za mara kwa mara.
Hayo yalisemwa jijini Dar es Salaam leo, wakazi hao wakati walipokuwa wakizungumza na BLOG hii katika eneo la Kimara Mwisho.
Kwa niaba ya wenzake, Charles Simon, alisema hawelewi kuna tatizo gani ambalo linafanya mafundi hao wawe wanabomoa vipande vya barabara hiyo vilivyokamilika.
“Unajua Watanzania sisi ni watu wa ajabu sana kila kinachofanyika kiwe ni kizuri au kibaya hakuna anayehoji, angalia barabara hii kuna maeneo yamekamilika kabisa lakini ghafla tunaona yanabomolewa na kusabisha usumbufu kwa watumiaji wake lakini tuko kimya,”alisema Simon.
Alisema, wanahitaji waelezwe kinachosababisha barabara hiyo kubomolewa mara kwa mara kunasababishwa na nini, pia wajue kama ni uzembe serikali inamchukulia hatua gani mkandarasi.
Aidha, alisema mkandarasi huyo kama ataachwa aendelee na utaratibu huo wa kujenga na kubomoa kunauwezekano ujenzi huo ukashindikana kukamilika kwa wakati hali itakayowafanya watumiaji wa barabara hiyo kuendelee kuteseka na msongamano unaojitokeza mara kwa mara.
Aliyataja baadhi ya maeneo yaliyokumbwa na ubomoaji huo kuwa ni yale ya Kimara Fire na Akiba (kwenye makutano ya barabar ya Morogoro na Bititi).
Katika hatua nyingine wakazi hao pia wameiomba serikali kutekeleza kwa vitendo katika kuwakamata baadhi ya madereva wa magari na bodaboda ambao wamekuwa wakijihusha na vitendo vya wazi vya kuharibu barabara hiyo.
Simon, alisema ni jambo la kushangaza kwa madereva hao kushindwa kuwa na uvumilivu pindi inapotokea foleni, wao huamua kupanda kwenye maeneo amabyo kisheria hayaruhusiwi kupita matokeo yake ni kuharibu barabara hiyo.

“Tumesikia mara kadhaa kuwa kila anayejihusisha na uharibifu huo atakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria lakini cha kushangaza uharibifu huo unaendlea lakini hadi leo hakuna hata dereva mmoja aliyekwisha kamatwa na kufikishwa kwenye vyombo hivyo vya sheria.

No comments:

Post a Comment