KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Thursday, 26 February 2015

VICOBA WAGAWANA FAIDA-MUHEZA

NA STEVEN WILLIAM
Muheza

WANAKIKUNDI 30 wa Michungwani Vicoba wilayani Muheza mkoani Tanga
wamegawana fedha za faida katika hisa zao walizowekeza  katika mzunguko  Milioni 7,037,000 mwaka huu 2015.

Sherehe hiyo ilifanyika juzi  katika ofisi za  Vicoba hivyo iliopo Michungwani wilayani Muheza ambapo pia ulifanyika uchaguzi wa viongozi wapya.

Akitoa taarifa ya Vicoba hivyo vya Michungwani mlezi wa kikundi hicho
Steven Mlaguzi alisema kuwa katika mzunguko wa kwanza waligawana faida
ya fedha  Milioni  1127166 mwaka 2010.

Mlaguzi ambae pia ni Diwani wa kata ya Genge wilayani hapa alisema kuwa mzunguko wa pili wa kugawana faida ya fedha ulifanyika mwaka 2011 ambapo waligawana Milioni 4,58,500.

Alisema kuwa mzunguko wa tatu ulifanyika mwaka 20013 waligawana fedha
za faida Milioni 3,508,390.

Mlaguzi alisema kuwa baada ya kugawana  faida hiyo walifanya uchaguzi
wa  kuchagua viongozi wapya.

Alisema kuwawalimchagua Mwenyekiti mpya Frola Bright,katibu Winfrida
Lugonzibwa,Mweka hazina Joice Mngoma na mjumbe wa benki Betrice
Mselem.

Malaguzi alisema kuwa wanakikundi hao waliongeza hisa zao kutoka
shilingi 5000 hadi shilingi 10000.

Alisema kuwa kikundi hicho kinamradi wa kukodisha matrubai na viti
katika sherehe mbalimbali na misiba kwa lengo la wanakikundi hao kuondokana na umasikini na kuboresha maisha yao.


No comments:

Post a Comment