KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday, 17 March 2015

BENKI YA STANBIC YARAHISISHA HUDUMA


BENK ya Stanbic Tanzania imezindua huduma za kibenki kwa njia ya mtandao wa kieletronikali HIVI KARIBUNI zinazowawezesha wateja kupata huduma kupitia simu za mkononi au kwenye kompyuta zao binafsi.

Uzinduzi wa huduma hii mpya ni mkakati wa kuwapatia huduma wateja kwa urahisi hususani wanaotumia simu za mkononi ikizingatiwa kuwa  utumiaji wa simu hizo umekuwa kwa kiwango cha asilimia 80 barani Afrika na unazidi kukua hali inayotia matumaini kuwa siku za usoni huduma za kibenki zitawafikia kirahisi wananchi wengi wanaoishi maeneo ya vijijini ambao wengi wao kwa sasa hawanufaiki na huduma za kibenki.

Kwa sasa mabenki na taasisi mbalimbali za kifedha zimeanza mkakati wa kusambaza huduma zake ili ziwafikie wananchi wengi zaidi hususani wanaoishi maeneo ya vijijini kupitia huduma za mtandao wa  kielectronikali, pia huduma hizi zinawarahisishia wananchi wanaoishi mijini kupata huduma za kibenki na kuepukana na kupoteza muda wao mwingi kupanga foleni kwenye mabenki wanapohitaji kupata huduma.

Benki ya kimataifa ya Stanbic ambayo asili yake ni barani Afrika kwa hapa Tanzania imeanza kutoa huduma hii mpya kwa wateja binafsi na wateja wa makampuni na itawarahisishia maisha wateja wake ambao wataweza kupata huduma  za kibenki na kufanya mihamala ya malipo wakiwa majumbani kwao ka katika sehemu zao wanazofanyia biashara.

Akizungumzia huduma hiyo mpya Farha Mohammed,Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Benki kwa njia ya mtandao wa Stanbic Tanzania amesema :
 “Tumeanzisha huduma hii kuwarahisishia  maisha wateja wetu ambao kwa sasa wanaweza kupata huduma kwa urahisi na huduma hii ni salama,inaaminika na ni rahisi kuitumia hata kama mtumiaji anaitumia kwa mara ya kwanza,tumedhamiria kuondoa usumbufu wa kupata huduma za kibenki kwa wateja wetu”

Alisema wanachotakiwa kufanya wateja ni kujisajili kwa njia ya mtandao kwa kutumia vitambulisho vyao vyenye maelezo yanayowahusu.
Baada ya kujisajili mteja anaweza kuangalio salio kwenye akaunti yake,viwango vya ubadilishanaji fedha za kigeni vya siku,taarifa za akaunti yake,kununua umeme wa LUKU ,kulipia ankra ya maji na kununua muda wa maongezi wa simu na kadhalika.


No comments:

Post a Comment