![]() |
| Mbunge wa Mbinga, Kayombo |
NA MWANDISHI WETU
MKOPO wa sh. bilioni
mbili uliotolewa na Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kwa wakulima wa zao la
Kahawa wilayani Mbinga, umesaidia kwa kiasi kikubwa wakulima hao kuongeza
uzalishaji na kukuza vipato vyao.
Mbunge wa Mbinga
Mashariki, Gaudens Kayombo, alieleza hayo mjini hapa jana alipozungumza na
waandishi wa habari.
“Asilimia 90 hadi 95 ya
wananchi wa wilaya ya Mbinga ni wakulima na mkopo huu umesaidia kukuza vipato
vyao kupitia zao la kahawa,”alisema.
Alisema mwaka jana
waliingia mkataba na NSSF na vyama vya msingi vinne kufanikiwa kupata mkopo
na kununua zao hilo kutoka kwa wakulima na ndani ya siku 100
walikamilisha kulipa mkopo huo.
Pia alisema mkopo huo
ulifuta mfumo holela wa ununuzi wa zao hilo
ambapo wakulima walikuwa hawapati faida ya kutosha.
Alizitaka kampuni za
watu binafsi zinazonunua zao hilo wilayani hapa
kuangalia wakati wa kununua zao hilo,
ili wakulima nao waweze kufaidika.
“Katika kipindi cha miaka tisa na zaidi kuna
maendeleo makubwa yamepatikana chini ya kaulimbiu ‘Mbinga Mbinguni’,” alisema
na kuongeza kuwa wanatarajia Mbinga iwe mfano wa wengine kuiga.

No comments:
Post a Comment