KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday, 17 March 2015

WAKAZI WA DAR WAMTAKA MAGUFULI ATOE UFAFANUZI KUHUSU UJENZI WA STENDI ZA DART

Waziri wa Ujenzi, John Magufuli
BAADHI ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam, wameitaka Wizara ya Ujenzi kutoa ufafanuzi kuhusu stendi za mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DART), kujengwa kwa kutumia mbao na nyavu kama vile mabanda ya kuku.
Wakazi hao, walisema hivyo kutokana na maelezo kuwa stendi za mradi huo zingejengwa kisasa zaidi kwa kutumia vioo na teknolojia inayokwenda na mfumo wa kidigital.
Walisema pamoja na matumizi hayo ya mbao, kibaya zaidi mbao hizo zinaonekana kuwa dhaifu na kwamba zinaweza kuharibika kwa muda mfupi.
“Tunaomba ufafanuzi mapema ili likija kutokea la kutokea wahusika wasije kukwepa ubadhilifu wanaoufanya, tumebaini katika hatua hizi za mwisho kuna maeneo yanajengwa chini ya kiwango mfano ni uwekwaji wa hizi mbao na nyavu ambazo hazifanani kabisa na mradi wenyewe.
 “Hapa tunahisi kuna ufisadi unafanyika kwa mtu asiyeamini hebu kuanzia sasa ajaribu kufuatilia mchezo unaofanywa na wakandarasi waliopewa kujenga hizi stendi,”alisikika mmoja wa wakazi hao.
Walizitaja baadhi ya stendi hizo kuwa ni zile za kuanzia Kimara mwisho ambazo ni Bucha, Baruti, Kona na nyigine.
Wakazi hao walisema wanawasiwasi kuwa huenda mipango iliyokusudiwa awali ikawa imeishaanzwa kuvurugwa na baadhi ya watu wenye taamaa ya fedha.
Waliendelea kusema kuwa ni vema Waziri wa Ujenzi John Magufuli akafanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo, kisha atoe ufafanuzi kama ujenzi huo ulipangwa kuwa wa aina hiyo,  itasaidia kuwatoa wasiwasi wananchi.


No comments:

Post a Comment