![]() |
| Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Mussa Natty |
DIWANI
wa Kata ya Saranga wilayani Kinondoni, Ephraim Kinyafu, amemtaka Mhandisi wa
Manispaa hiyo kutoa maelezo kutokana na kushindwa kuhamisha nguzo tisa za
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ili kupisha ujenzi wa barabara ya Saranga
Arsenal.
Kinyafu,
alisema Tanesco iliingia makubaliano kwamba kabla ya ujenzi wa barabara hiyo
kuanza Manispaa hiyo itafute mkandarasi wa kuhamisha nguzo hizo, ambaye gharama
zake ingezilipa.
Alisema,
sasa ni zaidi ya miezi mitatu nguzo hizo hazijahamishwa hali iliyoifanya
Kampuni ya Ujenzi wa Barabara hiyo Skol (SBC), kuwamua kujenga huku nguzo hizo
zikiwa robo tatu ndani ya barabara jambo ambalo ni la hatari.
Kinyafu,
alisema hayao jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, wakati alipofanya ziara
ya kushtukiza ya kukagua maendeleo ya mradi huo ambao ulianza mwishoni mwa
mwaka jana.
Alisema,
hivyo kwa vile aliwasiliana na Tanesco ambayo ilimjibu kuwa tatizo la
kuhamishwa nguzo hizo haliko kwao wanachosubiri wao ni utekelezaji wa malipo
kwa mkandarasi atakayepewa zabuni hiyo kama ilivyokubaliana awali na Manspaa
hiyo.
Kinyafu
alisema licha ya makubaliano hayo, hadi sasa hakuna taarifa ambazo zimetolewa
na ofisi ya mhandisi wa Manispaa hiyo kwamba ni sababu zipi zilizofanya
wachelewe kumpata mkandarasi wa kuhamisha nguzo hizo tisa.
“Hii ni hatari kwa nguzo za umeme kusimama
katikati ya barabara tunaweza kujakupata janga kubwa ambalo linaweza kugharimu
roho za watu na uharibifu wa mali na serikali kuingia gharama kubwa katika
kuwadumia waathirika,”alisema Kinyafu.
Msimamizi
wa Kampuni ya SBC, Efard Benson, alisema wameamua kujenga huku nguzo hizo
zikiwepo kwa sababu taratibu kwa upande wao zilikuwa zimekamiliaka tangu
mwishoni mwa mwaka jana na istoshe wanakwenda na wakati.
Alisema,
kama wangeendelea kusubiri kuhamishwa nguzo hizo ina maana hadi leo wangekuwa
hawajaanza ujenzi kitendo ambacho kingewaongezea gharama zisizo za lazima.
“Kweli uwepo wa nguzo zile ndani ya barabara ni
kikwazo pia tayari kumekwishatokea ajali mara mbili kwa magari kuzigonga na
kusababisha taharuki kwa nguzo hizo kuanguka barabarani pia wananchi kuosa
huduma hiyo kwa zaidi ya siku moja,” alisema Benson.
Benson,
alimuomba diwani, kwamba aendelee kutia msukumo katika kuhamishwa nguzo hizo
kwani tangu hiyo barabara ilipoanza kujengwa kwa kiwango cha lami magari mengi
yanapita, akibainisha kuwa uwezekano wa kutokea ajali ni mkubwa kama
hazitahamishwa haraka.

No comments:
Post a Comment