![]() |
| Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi |
MWENYEKITI wa Kijiji cha Nyakasangwe Kata ya Wazo
wilayani Kinondoni, Peter Mibilale anadaiwa kupora ardhi ya mkazi wa kijiji
hicho, Claud Chikonyi, kuingia katika makubaliano ya kuiuza kwa mtu ambaye
hakujua kama alikuwa akimchunguza.
Alisema, baada yakuporwa eneo lake aliwatafuta waandishi wa habari, ambao
walifanya uchunguzi kwa mmoja wao kujigeuza mteja anayetafuta eneo la kununua katika
kijiji hicho ndipo mwenyekiti huyo alipojitokeza na kuingia makubaliano ya
kuuza kipande hicho cha ardhi, alichodaiwa kukipora kwa Chikonyi.
“Nasikitika kama kiongozi aliyechaguliwa kwa nia ya
kusaidia kutatua matatizo yanayojitokeza katika jamii leo yeye ndiyoanakuwa
wakwanza kuwavuruga wananchi, sasa wananchi watakimbilia wapi watakakopata haki
zao,”alisema Chikonyi.
Ofisa Ardhi wa Manispaa hiyo, Jermia Masinga alisema
hakuna sheria inayomruhusu Mwenyekiti wa serikali ya mtaa kugawa ardhi, hata
kama serikali ikiamua kuchukua eneo la mwananchi lazima afidiwe.
Alisema wanaohusika kugawa ardhi ni Kamati ya Wilaya
ambayo Mwenyekiti wake ni Mkurugenzi huku Meya akiwa Katibu.
Masinga, alisema kama kweli mtu huyo amefikia hatua hiyo
basi achukuliwe kuwa ni mhalifu, anayedai kuporwa eneo lake achukue hatua za
kumfikisha kwenye vyombo vya sheria kama wahalifu wengine.
Hata hivyo, Mchungaji huyo alipogiwa simu na waandishi
hao na kuelezwa madai hayo alikata simu hata alipopigiwa tena simu iliita kwa
muda mrefu hadi kukatika yenyewe.

No comments:
Post a Comment