KAMPUNI
ya Mawasiliano na Masoko ya East Africa
Unique, inaandaa maonyesho ya uwekezaji
ili kuweka msukumo wa uwekezaji.
Maonyesho
hayo yatafanyika katika Hoteli ya Golden iliyopo jijini Dar es Salaam kuanzia
Mei 3 hadi Juni 4 Juni mwaka huu.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa
kampuni hiyo, Rodgers Mbaga alisema maonyesho hayo kampuni yake imepanga na
kuweka mikakati ya kuhakikisha biashara endelevu kwa kuandaa mafunzo ya
kuwajengea uwezo wenye miradi.
"Katika
maonyesho hayo mafunzo yatakayotolewa ni
pamoja na kutayarisha miswaada,
mapendekezo ya miradi ambayo inawavutia
wawekezaji na watoaji wa mitaji,"
alisema.
Mbaga
alisema mafunzo mengine ni uendeshaji wa miradi, usimamizi wa fedha na kufuata taratibu, uuzaji na utafutaji wa
masoko, mbinu za mawasiliano na namna ya
kushawishi wawekezaji na watoaji mitaji kukubali miradi inayopendekezwa.
Aliongeza
kuwa wataangalia namna ya kufikiri, kuongeza
upeo wa kulenga miradi ya
wastani isiyopungua dola za Marekani
laki mbili na nusu, kuwa waaminifu na kujituma kulingana na uwezo na ukomo wao.
"Watakaoshiriki
TIPEC ni sekta binafisi (TPSF), Baraza la
biashara la kitaifa (TNBC), Mamlaka ya
Export Processing Zone (EZPA), Mamlaka ya maendeleo ya biashara Tanzania
(TANTRADE), Taasisi za wenye viwanda na
biashara biashara (TCCIA) na Shirikisho la wenye viwanda Tanzania (CTI)," alisema.
Aliongeza
kuwa kuanzia mwaka 2016 TIPEC itatembelea nchi zisizopungua mbili
ili kukuza miradi ya mahususi ya biashara.
No comments:
Post a Comment