UMOJA wa Wafanyabiashara Walemavu Dar es Salaam (UWAWADA),
umemshutumu mmoja wa aliyewahi kuwa
Mwenyekiti wa umoja huo, David Nyendo, kujipatia mkopo wa sh milioni 500 kwa
kutumia Saccos ya walemavu.
Wakati Nyendo akishutumiwa, naye amefunguka akisema
wanaodai hivyo hawajui chochote kuhusu kunachoendelea katika upatikanaji wa
mikopo hiyo.
Nyendo, aliondolewa madarakani miaka mitatu iliyopita baada
ya kutokea vurugu kubwa za kupinga uongozi wake, hata hivyo, inadaiwa wakati anaondoka, aliondoka na baadhi
ya nyaraka za Saccos hiyo.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini leo, Mwenyekiti wa
Umoja huo Mohamed Kidumke, alisema kitendo alichofanya Nyendo ni cha kikatili
kwani anajua changamoto zinazo wakabili walemavu wenzake.
“Hii Saccos ilifungwa baada ya Saccos hiyo kuyumba hadi
kushindwa kuwaapatia mikopo wanachama wake pia pango la ofisi na kuzuiliwa
vyombo vyake na mmiliki wa nyumba,”alisema.
Alisema, mwaka jana Nyendo alitumia fojali kwa kuomba
mkopowa sh. 200 kwa kutumia nyaraka za umoja huo kwa maslahi yake binafsi
pamoja na rafiki yake.
Kidumke, alisema mkopo huo aliutumia kwa kunulia Bajaji na gari
ambazo hakuzitaja idai yake, alizozitumia kufanya biashara ya kusafirisha
abiria (Daladala).
Alisema kutoka na biashara zake hizo alifanikiwa kurejesha
mkopo huo kwa wakati, ambapo alichukuwa mwingine wa milioni 307.
Kwa upande wake Nyendo, alisema hao wamekosea, kwanza
wanaotoa madai hayao ni watu wachache ambao hawajui kinachoendelea.
Alisema mkopo unaotolewa na NSSF hautolewi kwa Saccos
Walemavu kama wanavyo dhani ni kwa ni wanachama wa sakosi hiyo ambao
wamechangia michango yao katika mfuko huo wa NSSF kwa zaidi ya miezi sita.
“Ili mwanachama atambulike ni lazima awe anachangia
michango yake kila mwezi na katika kupatiwa mkopo ni lazima iangaliwe kiasi
alichochangia pia mkopo huo utaenda na dhamana.
“Sijatumia fojali kama walivyosema, unajua baada ya Saccos
ile kuyumba mwaka 2012 ilibidi iundwe nyingine mwaka 2013 sasa cha msingi
wanachotakiwa ni kujiunga na sakosi hiyo na kuanza kuchangia NSS kupitia Saccos yetu,”alisema Nyendo.
Nyendo alisema katika mkutano kati ya Uwawada, Katibu
tawala wa Mkoa na Maofisa Ushirika wa Ilala na Temeke, walikubaliana kuwa wanachama
wa Uwawada kuanzia sasa waanze kujiunga
na Saccos hiyo kisha walipe michango yao, baada ya kutimiza miezi sita
wataangaliwa na wataalamu wa NSSF kama wametiza vigezo.
No comments:
Post a Comment