MMLIKI wa nyumba aliyokuwa akiishi
Mwalimu wa shule ya Sekondari Kibasila Gaudensia Albert aliyekutwa na mrundikano
wa kinyesi chumbani kwake, Reuben Shayo, amesema hajamuona mwalimu huyo tangu
kutokea tukio hilo mwezi mmoja uliyopita.
Tukio hilo limetokea katika mtaa wa
Kisiwani Kata ya Sandari wilayani Temeke jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na wandishi wa habari
jijini leo, Shayo alisema kutoonekana kwa mwalimu huyo hakumtii wa wasiwasi
kwani hadi sasa vyombo vyake viko katika hali ya usalama pia hana deni
analomdai.
Alisema, hivyo kwa vile haoni haja ya
kumtafuta mwalimu huyo kwani hana deni analodai ambapo hadi sasa mwalimu huyo
anamkataba wakuishi katika chumba hicho hadi Juni mwaka huu.
Alisema, baada ya kumalizika mkataba
wake kama hataonekana basi atatumia njia alizotumia awali za kuwatafuta
viongozi wa serikali ya mtaa na polisi ili kutoa vyombo vyake.
“Unajua hata tulipokiteketeza ule
mrundikano wa kinyesi kilichochanganyika na matapishi na mikojo ilibidi tuvunje
mlango kwa kutumia nguvu ya dola kwa ajili ya usalama wa vyombo vyake na
tulipomaliza kuvunja lilinunuliwa kufuli jipya ambalo ndio limebana mlango wa
chumba hicho cha mwalimu na funguo ziko kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo
Yahya Bwanga,”alisema Shayo.
Mkuu wa Shule Msaidi, Frida Kyando,
alipoulizwa kama mwalimu huyo anaonekana shuleni hapo, alisema tangu
zilipozagaa taarifa hizo alipatwa na mshtuko ambao umemfanya aplekwe hospitali
ya Temeke baadae kuhamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.
“Kwani mkataba wake wa kupanga hicho
chumba umeisha basi kama bado hakuna tatizo,:alisema Frida.
Frida, alisema hivi sasa mwalimu
Gaudensi bado amelazwa katika Hospitali hiyo, akidai kuwa yuko katika hali
mbaya.
Mwezi mmoja uliyopita katika chumba
anachoishi mwalimu huyo kuligundulika mlundikano wa kinyesi kilichokuwa
kimehifadhiwa katika ndoo za plastiki, mabeseni, chupa za chain a soda, na
vyombo vingine vyote vikiwa vimejaa kinyesi hicho kilichohifadhiwa kwa muda wa
miaka miwili.
No comments:
Post a Comment