KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Monday, 9 March 2015

MFUMUKO WA BEI WAPANDA KWA ASILIMIA MBILI

Mkurugenzi wa Takwimu za Jamii, Ephraim Kwesigabo
OFISI ya Taifa ya Takwimu (NBS),  imesema mfumuko wa bei wa Taifa umeongezeka kutoka asilimia 4.0 katika kipindi cha Januari hadi asilimia 4.2, Februari mwaka huu.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Takwimu za Jamii, Ephraim Kwesigabo, alisema Fahiri za bei zimeongezeka kutoka 148.62 Februari, 2014 hadi 154.83 kwa Februari mwaka huu.
Alisema hali hiyo imetokana na kasi ya upandaji wa bei za bidhaa na huduma kwa mwaka uliyoishia Februari mwaka huu, imeongezeka ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka uliyoishia Januari mwaka huu.
Kwesigabo, alitaja baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa fahirisi, zikiwa na asilimia yake ndani ya mabano kuwa ni pamoja ni mchele (5.0), samaki (3.0), matunda aina ya machungwa (7.7), ndizi za kupika (2.6) na mbogamboga (5.3).
Nyingine ni baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula ambapo zilichangia kuongezeka kwa fahirisi ni pamoja na mkaa (11.5), vyombo vya jikoni vya aina ya kioo (2.5) na vyakula vya migahawani (1.5).
Kuhusu thamani ya shilingi ya Tanzania
Kwesigambo, alisema thamani ya shilingi inatafriwa kuwa ni badiliko la uwezo wa shilingi ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma zilezile za mlaji ambazo shilingi hiyo ingeweza kununua katika vipindi tofauti
“Ikiwa wastani wa fahirisi za bei za taifa unaongezeka, uwezo wa shilingi ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma hupungua,”alisema Kwesigabo.

Aidha, alisema uwezo wa sh. 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma umeshuka hadi sh. 64.59 mwezi Februari mwaka huu kutoka Septemba mwaka 2010.

No comments:

Post a Comment