KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday, 22 March 2015

MkM YAANDAA MFUNZO YA SIKU MBILI YA WAKULIMA NA WAANDISHI


NA MWANDISHI WETU

MRADI wa mawasiliano kwa wakulima nchini unaojulikana kwa jina la Mkulima Mbunifu, unatarajia kutoa mafunzo ya Kilimo Hai, ya siku mbili kuanzia Machi 30 hadi 31 mwaka huu mkoani Arusha.

Kwa mujibu Msimamizi wa Mradi huo Tanzania, Ayubu Nnko, mradi huo unasimamiwa na Biovision Africa Trust, kwa ufadhili wa Shirika la Biovisior Foundation for Ecological Development, Switzerland.

Alisema mafunzo hayo ya siku mbili yatajumuisha wandishi wa habari za kilimo na mazingira pamoja na wadau wengine wa kilimo na ufugaji.

“Hawa ni wadau ambao kwa namna moja au nyingine wanashiriki katika kueneza na kutoa elimu ya kilimo endelevu nchini,”alisema Nnko.

Nnko, alisema katika kufikisha elimu kwa walengwa mradi huo unachapisha na kusambaza jarida la lijilikanalo kwa jina la Mkulima Mbunifu, pamoja na machapisho mengine kwa vikundi vya wakulima hapa nchini na baadhi ya maeneo ya nchi jirani zinazopakana na Tanzania.

Pia wanatayarisha vipindi mbalimbali vya redio vinavyorushwa kupitia Shirika la Utangazaji nchini TBC Taifa na Sauti ya Injili Moshi.

“Huduma hii hutolewa bure kwa vikundi vya wakulima na taasisi zinazojishughulisha na kilimo endelevu,”alisema Nnko.   


No comments:

Post a Comment