KAMPUNI
binafsi
inayoshughulikia mawasiliano ya habari kwenye mtandao wa televisheni ya
dijitali, Star times inakabiliana na changamoto za miundombinu
hafifu na umbali wa maeneo katika zoezi la kusimika mitambo.
Akizungumzia
suala hilo, Mkurugenzi wa Uhusiano wa Umma wa Kampuni hiyo, Zuhura Hanif alisema anaipongeza Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania (TCRA), kwa kuzima mitambo ya analojia ili kufanya
mabadiliko makubwa ya matangazo ya luninga na pia kuelezea changamoto
wanazokumbana nazo kama kampuni.
Alisema,
kampuni hiyo ipo katikia wakati mgumu wa kuwafikia wateja popote walipo kwani
huduma zao zinahitajika sana, hasa maeneo ya vijijini.
“Tanzania
ni nchi kubwa sana yenye ukubwa wa kilometa za mraba takribani laki tisa na
nusu, mikoa 26 na wakazi takribani million 44 kwa mujibu wa sensa ya watu na
makazi iliyofanyika hivi karibuni, hivyo tatizo kubwa tunalokumbana nalo ni
miundombinu hafifu na umbali wa maeneo hayo katika zoezi la kusimika mitambo
yetu kuwa mgumu kidogo lakini tunapambana kufanikisha hilo,”alisema Hanif.
Akizungumzia
hatua ya uzimaji wa mitambo hiyo, alisema Tanzania ni nchi ya kwanza barani
Afrika kuzima mitambo ya utangazaji wa luninga kwa mfumo wa analojia na kuhamia
dijitali, zoezi ambalo lilianza mapema mwa mwezi Disemba 31 mwaka 2013.
“Uzimaji
wa mitambo ya analojia ni fursa kubwa kwa watazamaji wa luninga kwani unawapa
matangazo bora na yenye uangavu tofauti na mfumo wa awali, pia matangazo hayo
watazamaji wanaweza kutazama chaneli na programu nyingi zenye maudhui
mbalimbali yenye kukidhi haja ya kila mmoja wapo,”alisema.
Hata
hivyo, Hanif alieleza kuwa kabla ya kuzimwa kwa mitambo hiyo, kulikuwepo na
changamoto kwa watazamaji kutokana na hofu juu ya masuala mbalimbali ambayo
walidhani yangeweza kukwamisha zoezi hilo.
“Wapo
waliofikiria Tanzania bado hatuko tayari kwani kiteknolojia tuko nyuma, uchumi
wetu ni mdogo, hakuna wawekezaji wa kutosha kutoa huduma hii, upatikanaji wa
visimbuzi, gharama kubwa za visimbuzi, elimu ya kutosha kwa watumiaji na
kadhalika, l
akini
tofauti na ilivyotarajiwa, mitambo ilizimwa na kwa awamu katika maeneo ambayo
yamewekewa miundombinu ya mfumo wa dijitali,”alisema.
Alieleza
kuwa mafanikio makubwa yameonekana katika maeneo ambayo mitambo ya analojia
ilizimwa na wakazi wake kuhamia katika dijitali, ambapo wananchi wameipokea
vizuri huduma hiyo kwani miundombinu ilikuwa tayari imekwishaandaliwa ili
kuondokana na usumbufu wa aina yeyote.
“Kwetu
sisi kama wawekezaji zipo changamoto ambazo tumekumbana nazo na tunaendelea
kukumbana nazo, lakini kwa ushirikiano wa karibu na serikali mambo yanakwenda
vizuri,”alisema.
No comments:
Post a Comment