| | |
KUTOKANA na
kukithiri kwa ajali za barabarani nchini zilizosababisha vivyo vya takriban watu
1,000 waandaaji wa kipindi cha Mada Motto kinachorushwa katika kituo cha
Channel Ten, wameamua kuandaa kipindi maalumu leo kitakachotafuta ufumbuzi wa
tatizo hilo.
Akizungumza katika
taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari, mwandaaji wa kipindi hicho ambacho
zamani kiliitwa Kitimoto, Ally Oki alisema walikuwa na mada nyingine kwa
Jumatatu lakini wameamua kuiweka pembeni ili kuleta kipindi hicho maalumu.
Aidha,
katika kipindi hicho watahusishwa madereva na wadau wa usafiri ili kujua chanzo
cha ajali hizo ni nini hasa ikizingatiwa sekta ya usafirishaji inachangia
asilimia kubwa ya pato la taifa.
“Ndugu zetu
wengi wanapoteza maisha barabarani, wengine wanajawa na hofu hata kuahirisha
safari zao kutokana na taarifa za ajali kila siku. Kuna tatizo linalohitaji
ufumbuzi wa kudumu, tunaweza kuanza kwa kuwasikiliza madereva wana nini.
“Huwezi
kujua inawezekana wana mambo mengi vichwani mwao hawana pa kusemea, lakini watu
wa serikali tutakuwa nao na watakaoshindwa kuja wataungana nasi kwa njia ya
simu, lakini majibu lazima yapatikane,” alisema Oki.
Aliongeza kuwa
katika kipindi icho kinachorushwa mara tatu kwa wiki kuanzia saa nne mpaka saa
tano kwa leo kitarushwa kwa saa moja na nusu kutokana na umuhimu wake.
“Tangu
tuanze kipindi wiki iliyopita tumekuwa tukitumia muda wa saa moja, kwa siku za Jumatatu,
Jumatano na Ijumaa lakini kutokana na umuhimu wa suala hili la ajali tumeongeza
nusu saa ili watu wapate muda mwingi wa kueleza mawazo yao,” alisema.
Alisisitiza kuwa
kwa wale watakaokuwa mbali na luninga wanaweza kuchangia wanweza kutoa mawazo
yao kwa njia ya mtandao wa kijamii facebook na tittwer aau tovuti ambazo ni
(madamottotvshow/facebook , @madamottotvshow/twitter na www.madamottotvshow.com).
Mpaka sasa
kipindi hicho kimesharusha mada nne ambazo ni ajali za barabarani, mswada wa
makosa ya mtandaoni (Cyber Crime), kwanini Tanzania masikini na namna gani
tunakabiliana na maafa.

No comments:
Post a Comment