![]() |
| Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara, Minja |
MAHAKAMA ya Wilaya ya
Dodoma imeahirisha kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Wafanyabiashara nchini, Johnson Minja hadi Mei 7 mwaka huu kutokana na upande wa serikali kutokamilisha
uandaaji wa maelezo ya awali.
Ombi la kuahirishwa
kesi hiyo lilitolewa jana na Wakili wa Serikali, Rose Shio, wakati kesi hiyo
ilipofikishwa mahakamani hapo.
Baada ya kuwasilishwa
kwa ombi hilo, Wakili wa mshtakiwa, Godfrey Wasonga, alisema hana pingamizi,
hivyo Hakimu Mfawidhi, Rhada Ngimilanga kuahirisha kesi hiyo hadi Mei 7 mwaka
huu.
Minja ambaye yupo nje
kwa dhamana, katika kesi hiyo anakabiliwa na mashtaka mawili ya kuwachochea
wafanyabiashara kutenda kosa na kuwazuia kulipa kodi kwa kutumia mashine za
kielektroniki za (EFD’s).

No comments:
Post a Comment