KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday, 7 April 2015

MGEJA AWASHANGAA VIJANA WAZALENDO WA CCM



Mjumbe wa Halmashauri Mkuu CCM Taifa, Mgeja

MJUMBE wa Halmshauri Kuu ya CCM Taifa, Khamis Mgeja ameliita kundi la vijana wa zalendo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwa ni genge la vijana linalotumiwa kwa malengo ya mtu aliyewatuma.
Mgeja alitoa kauli hiyo baada ya kushtushwa na vijana hao wanaojiita wazalendo wa CCM kutoka Tanzania Bara na Visiwani, kutoa tamko ambalo linadai kuwa baadhi ya makada wanaotaka kuwania nafasi ya urais kuonyesha kiburi cha kutofuata sheria na kanuni za chama licha ya kuonywa mara kwa mara.
Makada hao, ambao wameonywa na kupewa adhabu ya miezi 12 kwa kuanza kampeni mapema, Februari 18 mwaka jana ni Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Steven Wasira, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba, Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja na mawaziri wakuu wastaafu, Edward Lowassa na Frederick Sumaye.

“Wao wanapodai kuna makundi ndani ya chama kwa kauli hiyo basi nao wajue tayari wamekwishaanzisha ubaguzi, ila wajue makundi wakati wa uchaguzi ni jambo kawaida ili mradi hayahasimiani, pindi uchaguzi unapokwisha nayo hutoweka,”alisema Mgeja.

Megeja, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, alisema hivyo kwa vile genge hilo ndani ya chama haliko kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.

“Genge hilo ni la watu, unaona bwana, hawa ni vijana ambao wamekuswanywa wakitumiwa kwa malengo ya mtu yaliyewatuma, tunajuana hawa wanatumika kinyume na maelezo yao,”alisema Mgeja

Alisema chama ni vikao kama wao wanaagenda yao nzuri waiwasilishe kwenye vikao halali vya chama lakini cham hakiwezi kujengwa na agenda za watu ambao hawajulikani.

“Kitendo wanachotumia ni sawa na kumtishia mtu mzima nyau hao waache kuwatishiwa watu wazima nyau, wao kama wana ubavu na hoja waseme lakini wajue chama kuanzia ngazi chini hakina mgongano, wasiwape hofu wanachama nchini,”alisema Mgeja.

Alisema kama kweli wao ni wazalendo basi watumie nguvu zao kueneza mazuri yaliyofanywa na chama chao chini ya Rais Jakaya Kikwete, lakini siyo vyema wakadandia treni wasilolijua.

Mgeja, aliwataka vijana kutambua kuwa chama hakiwezi kujengwa nje ya chama hivyo ni vema vijana hao wakajenga hoja zao kisha waziwasilishe katika vikao halali, akiamini kuwa watasikilizwa.

Alisema ni jambo la hatari kwa baadhi ya wanachama kuanzisha makundi kama hilo la wazalendo ndani ya chama kitendo hicho kinaweza kuleta mpasuko wa chama jambo ambalo haliombei.

“Kwa kuwa na kundi la wazalendo na kundi ambalo sio wazelendo hili ni pepo baya kwa mustakabali wa chama, linafaa likemewe,”alisema Mgeja.

Hivi karibuni Mwenyekiti wa vijana wa zalendo wa CCM, Hassan Marijan, alikaririwa na vyombo akisema kuwa wameshuhudia kundi fulani la makada ambao wanatumia mwanya wa kuwashawishiwa kugombea Urais.

Alisema makada hao wamekuwa wakiandaa makundi mbalimbali ya kijamii kwa mkono wa fedha ili mkakati wao, kwa kutumia umasikini na shinda za Watanzania kwa lengo la kujinufaisha.

No comments:

Post a Comment