KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday, 7 April 2015

MWANACHUO MJAMZITO ANUSURIKA BAADA YA KUJIDAI AMEKUFA

Mwanachuo Milicent Murugi akiongeaa na wanahabari Picha na Jeff Angote
 Mwananfunzi mmoja Milicent Murungi wa chuo kikuu cha Garissa ambaye ni mjamzito wa miezi nane amesema ilibidi ajifanye amekufa baada magaidi wa Al Shabab kuvamia Chuo Kikuu cha Garissa na kuua wanachuo wasiokua na hatia.

Akizungumza na wandishi wa habari jijini hapa, Milicent Murungi, alisema ilibdi atumie mbinu hiyo ili mchukuwa kwa saa 10 baada ya kubaini wenzake waliokua nao kwenye chumba hicho kuawa.

Milicent, alisema baada ya kubaini hivyo alijipakaza damu ya mmoja ya wanafunzi aliyeuawa, kujipaka kichwani wakati huo wapiganaji hao wa Al Shabaab walisikika wakielekea vyumba vya juu na kumbakiza mmoja pale chini alipokuwepo.

Milicent Murungi kutoka Embu na mwanafunzi wa mwaka wa pili katika chuo hicho cha Garissa alisema taratibu alichukua damu na mwanachuo mwenzake aliyekua amekufa jirani yake na kujipaka kichwani na kujifanya amekufa kwa saa 10.

No comments:

Post a Comment