KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday, 7 April 2015

NPS YATAHADHARISHA WAKAZI WA JIJI KUHUSU MATAPELI WANAOWATAPELI WANANCHI

Mkurugenzi wa wa kampuni ya NPS, Hassan Khan
UONGOZI inayojishughulisha na uegeshaji wa magari ya Taifa, National Parking Solution (NPS) imewataka wakazi wa jiji la Dar es Salaam kuwa makini na baadhi ya watu wanaotumia vibaya jina la kampuni hiyo na kuwatapeli wananchi.

Mkurugenzi wa wa kampuni hiyo, Hassan Khan alisema, kumekuwepo na baadhi ya watu wanaojifanya ni wafanyakazi wa kampuni hiyo na kuwatapeli wanananchi pale wanapowakamata kwa kukiuka taratibu za maegesho ya magari.

Alisema tangu kusitishwa na kwa mikataba ya baadhi ya kampuni  zilizokuwa na tenda na halmashauri za Dar es Salaam ya kukamata watu wanaoegesha magari kimakosa, kumeibuka watu wanaojifanya kuwa ni watumishi wa kampuni hiyo na kuwatapeli wananchi.

Khan, alisema pamoja na kujifanya maofisa wa kampuni hiyo, watu hao huwaomba fedha wananchi wanaowakamata kwa kigezo cha kutowapeleka katika mamlaka zinazohusika jambo ambalo linasababisha usumbufu kwa wananchi.

“Kikubwa tunawaomba wananchi  wawe makini na ikibidi wawaulize maswali mengi watu pindi wanapowakamata na uzuri wafanyakazi wetu wote wana sare maalumu zinazowatambulisha,” alisema Khan.

Aidha, alisema tangu kampuni yake ianze kusimamia shughuli za uegeshaji magari katika jiji la Dar es Salaam hawajawahi kupokea malalamiko kuhusu ukiukwaji wa taratibu mbalimbali, jambo ambalo alidai kuwa linawapa nguvu katika utengdaji kazi wao.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki aliziagiza  halmashauri zote za mkoa huo kusitisha mikataba na kampuni za udalali baada ya kuwepo kwa malalamiko mengi kutoka kwa wananchi .

Alisema, lengo la kufanya hivyo ilikuwa ni kuwaondolea usumbufu  wananchi .

No comments:

Post a Comment