KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday, 7 April 2015

POLISI WAKISHIRIKIANA NA MGAMBO WA JIJI KUMPANDISHA MACHINGA KWENYE GARI KWA STAILI YAKE



Askari wa jiji wakishirikiana na Polisi Jamii kumpandisha kwa nguvu katika gari mfanyabiashara wa kuuza nguo katika Mtaa wa Mkwepu - Posta Mpya, jijini Dar es Salaam jana, kitendo ambacho kimelaaniwa na watu walioshuhudia tukio hilo kutokana na mmoja wa askari hao kuwatishia kwa bastola waandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima. (Picha na Fransisi Dande)

 
VITENDO vya kikatili vya kupigwa na kunyang’anywa mali za wafanyabiashara mbalimbali kwa kisingizio cha kusafisha jiji na kugawana badala ya kupeleka kunakoruhusiwa vimezidi kujitokeza jijini Dar es Salaam.

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda aliwahi kuagiza kuwa wakuu wa mikoa na wilaya kukaa na wafanyabiashara na kuangalia njia nzuri ya kufanya biashara ili kuondoa vurugu baina yao na vijana.
 
Pinda aliyasema hayo Januaari mwaka huu katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu alipojibu swali la Mbunge wa Ilala, Iddi Zungu (CCM) aliyetaka kujua kauli ya Serikali kuhusu polisi na wanamgambo wanaotumia nafasi ya kusafisha jiji kuwanyanyasa wafanyabiashara na kugawana mali zao.
 
Amesema yeye binafsi alitumiwa picha ya watendaji hao wakigawana mali walizowanyang’anya wafanyabiashara wakiwamo mamalishe, jambo ambalo ni kuwanyanyasa na kuwarudisha nyuma kimaendeleo.
 
Waziri Mkuu alikemea kitendo cha watendaji wa jiji na mikoa kutumia kusafisha jiji kunyanyasa wananchi.
 
Hivyo aliagiza wakuu wa wilaya na mikoa kukaa na wafanyabiashara ndogo na kupanga jinsi ya kuendesha biashara kistaarabu ikiwa ni pamoja na kupanga masoko ya jioni na Jumapili ili wafanye biashara muda mfupi na kuondoka.

Wakati Pinda akiagiza hayo Jeshi la Polisi wakishirikiana na mgambo katika mtaa wa Mtaa wa Mkwep na Makunganya jijini jana, walitembeza kipigo kwa wamachinga kwa madai kuwa walikuwa wakifanya biashara katika maeneo yasiyo rasmi.

Kwa mujibu wa mashuhuda, askari hao wakiwapiga wamachinga hao ambao walikuwa wakitii sheria kila walipoelekezwa.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo alisema askari hao waliyokuwa wameshika bastola na bunduki waliwavamia wafanyabiashara hao na kuanza kukusanya bidhaa zao na kuzipakiza katika gari bila ya kuziorodhesha kama inavyotakiwa.

Mashuhuda hao walisema baada ya kuona vitendo hivyo vya kikatili walianza kuwazomea askari hao ndipo akasikika kauli ya mmoja wa askari akimuelekeza kuwa apige risasi ili kuwanyamazisha wasizomee.

Hata hivyo, askari aliyekuwa akielekezwa alibaki kuhangaika akiwatafuta watu waliokuwa wakizomea kwani hakuweza kuwaona kwa vile walikuwa wakishuhudia tukio hilo wakiwa gorofani.
Sisi tukio lile lilikuwa halituhusu lakini kilichotukera ni kuona askari ambaye anategemewa kuwa  mlinzi wa amani leo yeye ndio anakuwa wakwanza kuvunja amani kwa kuwapora wananchi mali zao tena kwa kutumia vitisho vya silaha na kipigo bila huruma,”alisema mmoja wa mashuhuda hao.

Mashuhuda hao wametoa rai kwa serikali kuwa makini na vitendo vinavyofanywa na askari pindi wanapokuwa kazini kwa baadhi yao siyo waaminifu, vitendo hivyo vikiachwa viendelee uhusiano kati ya raia wao utakuwa mbaya.

Mbunge wa Ilala (CCM), Iddi Zungu, amekuwa mstari wa mbele katika kupambana na vitendo vya baadhi ya wanamgambo na polisi wanaotumia nafasi zao vibaya kwa kuwanyasa na kuwanyang’anya mali zao wafanyabiashara na kuzigawana mali hizo.

No comments:

Post a Comment