NA
MWANDISHI WETU
MWANACHAMA
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (Chadema), Muhima Singu, ametangazania ya
kugombea ubunge katika Jimbo la Shinyanga Mjini, linaloshikiliwa na Stephen
Masele wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Singu,
ambaye ni msomi wa Chuo Kuu na mfanyabiashara, alisema kutangaza kwake nia ya
kugombea nafasi hiyo kumetokana na nchi kuwa katika maandalizi ya Uchaguzi Mkuu
unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Miongoni
mwa maandalizi hayo ni pamoja na uboreshaji wa daftari la mpiga kura kwa ktumia
mfumo wa kieletriniki (BVR), huku Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wakidai
Tume huru itakayosimamia uchaguzi huo.
Akizungumza
na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Singu, alisema kuwa anawaomba
wananchi wa jimbo hilo, kumchagua yeye wakati utakapowadia ilia je kushirikiana
nao katika kuleta mapinduzi ya maendeleo ya jimbo hilo ambalo wambunge
waliopita wa CCM wameshindwa kufanya hivyo.
Alisema
endapo atafanikiwa nia yake hiyo, atahakikisha kuwa mgawo wa mapato yanayotokana
na rasilimali zote zilizoko katika mkoa huo zinagawanywa sawa kwa wananchi wote
bila kubagua.
“Shinyanga
ni mkoa waenye migodi mingi ambapo mingine ni ya miaka mingi lakini inashangaza
kuwa mgawo wa mapato yanayotokana na uuzwaji wa madini haujaleta mabadiliko ya
kiuchumi kwa wananchi kwa zaidi ya miaka 50 tangu nchi ijitawale,”alisema
Singu.
Alisema
wakazi wa jimbo hilo wanakabiliwa na umasikini wa kutisha kwani vijana wengi
hawana ajira kutokana na ajira nyingi katika migodi kushikwa na wageni.
“Haya
nitayapatia ufumbuzi kwa kuzingatia umakini wa sera bora za chama chetu,
ambacho kimejipanga kuwakomboa wananchi kutoka katika lindi la
umasikini,”alisema Singu.
Hata
hivyo, alisema yapo baadhi ya masuala ya kijamii ambayo yako ndani ya uwezo
wake kwa kushirikiana na wananchi atayapatia ufumbuzi.
Aidha,
alisema kuwa atashirikiana na taasisi zote za kijamii ikiwemo za dini ambazo
ziko karibu zaidi na jamii katika kutoa elimu ya ni muhimu
No comments:
Post a Comment