KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday, 3 May 2015

AISHA: MWENYEKITI TATUA MIGOGORO KWA KUZINGATIA SHERIA NA HAKI


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

DIWANI wa Kata ya Somangila Aisha Mpanjila, amemtahadhalisha Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbutu, Kigamboni wilayani Temeke jijini Dar es Salaam, ahakikishe anaitafutia ufumbuzi migogoro ya ardhi kwa kuzingatia sheria na haki.
Aisha, aliitoa kauli hiyo jijini juzi, wakati wa mkutano wa hadhara ambao ulifanyika viwanja vya kijiji hicho, ulitawaliwa na malalamiko yanayohusu migogoro ya ardhi ya muda mrefu.
Alisema hivyo, kwasbabu kama atashindwa kutatua migogoro hiyo kwa kuzingatia sheria na haki basi atambue kuwa itamueka katika mazingira magumu na itamshinda kitendo kitakachofanya wananchi washindwe kuwa na imani naye.
Aisha, alisema mfano wa migogoro hiyo ni ule wa shamba la Kijangwamiya, ambao bado unaonekana kuwachanganya wanakijiji kwamba hadi sasa hawamjui mmiliki halali wa shamba hilo.
 “Ukiangalia utaona kuwa suala la mgogoro wa shamba hilo la kijiji cha Kijangwamiaya halijapatiwa ufumbuzi kutokana na wananchi kuuliza maswali kuwa shamba hilo ni lao au ni la nani,”alisema Aisha.
Alisema kwa vile bado kuna maswali mengi kutoka kwa wananchi kuhusu shamba hilo basi ni vema akaendelea kulishughulikia kisheria ili ukweli ujulikane kuwa ni nani mmiliki halali.
Naye Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Jamal Mfaume, alisema wakati anaingia katika uongozi wa kijiji hicho, alikabidhiwa nyaraka ambazo zinaonesha kuwa shamba hilo ni la kijiji hicho.
“Unajua mimi nimeingia ni kakuta mikataba mbalimbali amabyo ilikuwa imeishaingiwa kisheria na uongozi uliyopita hivyo unaweza kuona kinachoendelea hapa,”alisema Mfaume.
Mafaume, alisema wakati anaingia katika uongozi amekuta migogoro mingi ya ardhi ambayo baadhi yake iko mahakamani hata hivyo, aliahidi kuwa ataishughulikia kwa kuzingatia sheria na haki.
Aidha, mkutano huo ulitawaliwa na itikadi za vyama jambo ambalio limfanya mmfanya mmoja wa wanankijiji hicho, Yeiko Nyerere, kuwatahadharisha wenzake kuwa waache kuchanganya masuala ya maendeleo na siasa.
Alisema kama wanakiji hao wataendekeza mihemuko ya kitikadi ya vyama vyao basi watambuwe kuwa maendeleo katika kijiji hicho yakuwa ndoto kwao.

No comments:

Post a Comment